0
Michuano ya Mapinduzi Cup inatarajiwa kuendelea kutimua vumbi hii leo katika uwanja wa Amani Visiwani Zanzibar kwa kupigwa michezo miwili majira ya saa 10:30 jioni na saa 2:30 usiku


Mchezo wa awali unaotarajiwa kupigwa majira ya saa 10:30 za jioni utawakutanisha mabingwa watetezi wa michuani hiyo URA kutoka nchini Uganda dhidi ya  washika bunduki wa KVZ kutokea hapa Zanzibar
Timu ya URA inayomilikiwa na  Mamlaka ya mapato nchini Uganda walitwaa ubigwa wa kombe  la mapinduzi kwa mara yao ya kwanza mwaka 2016 baada ya kumfunga mtibwa Sugar  mabao 3-1 katika hatua ya fainali January 13 mwaka 2016
Kikosi cha timu ya URA kilichotwaa ubigwa wa mapinduzi 2016

Mabao hayo ya URA yalifungwa na Julius Ntamb na Peter Lwasa aliyefunga magoli mawili katika dakika 85 na 88 huku bao pekee la Mtibwa  na la kufutia machozi likifungwa na Jaffar Salum na kuifanya URA kutwaa kitita cha shilingi milioni 10 za kitanzania

Mchezo huo  utakaopigwa mapema hii leo utakuwa ni mchezo wa pili kuchezwa tangu kufunguliwa rasmi kwa mashindano hayo desember 30  nna Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Omar Hassan King ambae alikuwa mgeni rasmi 

Mchezo wa pili utapigwa majira ya saa 2:30 usiku kwa kuzikutanisha Simba ya Dar es Salaam na Timu ya Taifa
Jang;ombe ambae ndio kinara wa kundi A
Ratiba ya michezo mengine ya Mapinduzi Cup  hiyo hapo chini 

RATIBA MAPINDUZI CUP .

 1/1/2017 KVZ VS URA Saa 10:00 alasiri, Simba vs Taifa ya Jang'ombe saa 2:30 usiku.
 2/1/2017 Azam vs Zimamoto saa 10:00 alasiri,Yanga vs Jamhuri saa 2:30 usiku.
 3/1/2017 Jang'ombe boys vs URA saa 10:00 alasiri,KVZ vs Simba saa 2:30 usiku.
 4/1/2017 Zimamoto vs Yanga saa 10:00 alasiri, Jamhuri vs Azam saa 2:30 usiku.
 5/1/2017 KVZ vs Jang'ombe boys saa 10:00 alasiri, Simba vs URA saa 2:30 usiku.

6/1/2017 Taifa ya jang'ombe vs KVZ saa 2:30 usiku.
 7/1/2017 Jamhuri vs Zimamoto saa 10:00 alasiri, Yanga vs Azam saa 2:30 usiku.
 8/1/2017 Simba vs Jang'ombe boys saa 10:00 alasiri ,Taifa ya jang'ombe vs URA 2:30 usiku.
 10/1/2017 Saa 10: 00 nusu fainal ya kwanza , Saa 2:30 nusu fainal ya pili.

13/1/2017 FAINAL saa 2: 30 usiku.

Post a Comment

 
Top