Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo akizungumza baada ya kuridhishwa na utendaji wa kazi ya ujenzi wa madarasa ya shule ya msingi Chang’ombe ‘A’ na ukarabati wa majengo ya shule wakati wa ziara aliyoifanya katika shule hiyo Januari 11,2017.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo akitoka kukagua ujenzi wa choo cha walimu katika shule ya msingi Chang’ombe ‘B’ wakati wa ziara yake aliyoifanya katika kata ya Chang’ombe.
Naibu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Seleman Jafo akiwa na mwanafunzi George John wa darasa la
saba ambaye ni mlemavu na kutoa agizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi,kuhakikisha
mradi wa ujenzi wa vyoo vya wanafunzi Shule ya Msingi Chang’ombe 'A'
unazingatia miundombinu rafiki kwa ajili ya watu wa ulemavu wakati wa ziara yake aliyoifanya katika kata ya Chang’ombe.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akipokea maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi waHalmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi juu ya ukamilifu wa ujenzi wa choo cha walimu shule ya msingi Chang’ombe ‘B’ pia uendelevu wa ujenzi wavyoo vya wanafunzi katika ziara yake aliyoifanya katika kata ya Chang’ombe.
.....................................................................................................
Naibu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo amewaagiza Wakuu wa wilaya
nchini kuhakikisha wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha
kwanza mwaka huu wanakwenda kuanza shule huku akiwasisitiza wazazi
watakaoshindwa kuwapeleka shule watoto hao wachukuliwe hatua za
kisheria.
Jafo
ametoa agizo hilo Januari 11,2017 alipofanya ziara ya kukagua miundombinu
mbalimbali katika shule za msingi, Chadulu, Chang’ombe A na B, Manispaa
ya Dodoma.
Katika
ziara yake ya kukagua maagizo aliyoyatoa kwenye shule hizo kuhusu
masuala ya miundombinu, Jafo amesema “Sisi kama serikali hatutaki mtoto
akose elimu hasa katika kipindi hichi ambacho serikali imeamua
kuelekeza nguvu za kutosha kwenye elimu kwa ajili ya watanzania.”
Ameongeza
“Kwa mzazi ambaye mtoto wake atabainika hajaenda shule na kupewa kazi
zingine kama kuendesha bodaboda hatua za kisheria zichukuliwe mara
moja,”.
Pamoja
na hayo, Jafo amekemea tabia ya wazazi kutotilia mkazo masuala ya elimu
na kuwakabidhi watoto wao kuendesha bodaboda kama ajira yao badala ya
kuwapeleka shule na kuwataka kuhakikisha wanawanunulia mahitaji yote ya
shule.
Aidha
amesema serikali haitarajii kuna vijana waliochaguliwa wakishawishiwa
na wazazi kufanya vibaya kwenye mitihani kutokana na elimu kuwa ni bure.
Akizungumzia
kuhusu watoto walioandikishwa kuanza kusoma elimu ya awali na msingi,
Jafo amesema kumekuwepo na mwitikio mkubwa katika suala la uandikishaji
watoto hao na linatokana na uwepo wa elimu bure.
Hata
hivyo, amesema shule nyingi idadi ya wanafunzi imeongezeka zaidi na kwa
serikali ni faraja kuona watanzania wengi sasa wanapata elimu huku
akiwataka wazazi wahakikishe watoto walioandikishwa wanahudhuria shule
ipasavyo na wakurugenzi kuendelea kuweka mazingira bora ya kujifunzia
na kufundishia.
Kadhalika,
Jafo ameridhishwa na ukarabati wa miundombinu mbalimbali kwenye shule
hizo huku akiwaahidi walimu kuwa serikali itaendelea kuboresha mazingira
ya kufundishia ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Naye,
Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma, Godwin Kunambi, amesema kwasasa
Manispaa hiyo inaendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwa ni
pamoja ujenzi wa shule za msingi na sekondari na kuongeza madarasa
kwenye baadhi ya shule ili kukabiliana na ongezeko la wanafunzi hasa
wanaohamia Dodoma.
Kwa
upande wake, Ofisa Elimu wa Manispaa hiyo, Scholastika Kapinga, amesema
hadi sasa watoto zaidi ya 8,000 wameandikishwa kwenye manispaa hiyo
kuanza kusoma elimu ya awali na msingi.
Post a Comment