Mkuu wa mkoa wa LIndi Godfrey Zambi akizungumza kwenye mahafali ya tatu ya VETA LINDI
Waandishi wetu
WADAU
mbalimbali wa maendeleo mkoani Lindi,wameombwa kuwahamasisha vijana wakiwemo wa
kike kujiunga na vyuo vya ufundi, kikiwemo cha Veta,ili wapate utaalamu
utakaowasaidia kuendesha maisha yao ya sasa na baadae.
Ushauri
huo umetolewa na mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi na huduma mkoani humo,Samwel
Ng’andu alipokuwa anatoa taarifa ya utekelezaji, kwenye mahafari ya tatu ya
wahitimu 108,yaliyofanyika viwanja vya Chuo hicho kilichopo mjini Lindi.
Akiwasilisha
taarifa hiyo,ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa mkoa huo,Godfrey Zambi,Ng’andu
alisema tangu Chuo hicho kianzishwe kutoa mafunzo miaka minne iliyopita,idadi
ya waschana kujiunga na Chuo sio ya kuridhisha,ikilinganishwa na mikoa mingine
hapa nchini.
Ng’andu
alisema tangu kuanzishwa kwa Chuo hicho cha Veta mwaka 2012,kimeweza kudahili
wanafunzi 1,122 kati yao wavulana 834 na waschana 279 sawa na asilimia 24.5%.
Alisema
kila mwaka Chuo hicho kinadahili wanafunzi ambapo kwa mwaka huu
2016,waliodahiliwa ni 280 kati yao waschana (29) tu,na kufanya waschana wote
waliokwisha dahiliwa tangu kuanzishwa kwa Chuo hicho,miaka miaka mitano
iliyopita kufikia waschana 65,idadi ambayo sio ya kuridhisha ndani ya mkoa huo.
Mkuu huyo wa Chuo cha Veta Lindi
alisema ndani ya kipindi cha miaka minne, kuanzia mwaka 2013 hadi
2016,kimeshatoa mafunzo kwa washiriki wapatao 1,497 wakiwemo wanaume 1,366 na
wanawake 131 sawa na asilimia 9%,idadi ambayo ni ndogo ikilinganishwa na uwezo
wa Chuo.
“Mh,mgeni
rasmi Chuo chetu cha Veta hapa Lindi,kina
uwezo mkubwa, lakini tatizo lililopo ni idadi ndogo ya watu kujitokeza kujiunga
nacho”Alisema Ng’andu.
Akizungumza
wakati wa mahafari hayo ya tatu,mkuu wa mkoa wa huo, Godfrey Zambi,amewataka
wananchi kuchangamkia fursa hiyo,kupata mafunzo ya ufundi Stadi kupitia Chuo
cha Veta cha Lindi,huku akipongeza jitihada zinazofanywa na viongozi kuweza
kupanua wigo wa mafunzo.
Zambi
pia amewataka wahitimu hao 108,kuwa mabalozi wazuri wanaporejea uraiani,ikiwemo
kuyatumia mafunzo waliyoyapata kwa kujiajili wao wenyewe,ili kujiletea
maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
Chuo
cha ufundi Stadi na huduma (Veta) mkoani Lindi,kilizinduliwa Apri 10/2012 na
aliyekuwa makamu wa Rais wa Tanzania awamu ya nne,Dakta Mohamedi Gharib
Bilali,kinaendesha fani mbalimbali, zikiwemo useremala,umeme,uunganishaji
vyuma,uhaziri,ushonaji na utengenezaji wa magari.
Post a Comment