Mojawapo ya kikwazo kingine kikubwa cha mafanikio katika
maisha ya mtu, ni tabia ya kusikiliza wanachoongea watu wengine juu yake
hata kama hakina ukweli wa maana ndani yake. Kama unataka kufanikiwa ni
vizuri ukajifunza kuheshimu kwanza mawazo yako uliyonayo yanayokupa
msimamo juu ya ndoto yako kabla ya mawazo ya nje. Usikubali mawazo ya
wengine kuwa namba moja kukukwamisha katika safari yako ya mafanikio.
Hii ndio maana unapaswa kuwa makini katika kuchagua ni watu gani wa kuwa
nao katika maisha yako, tafuta watu chanya wenye kuweza kukupa hatua
dhidi ya maono yako uliyonayo.
Jifunze kusikiliza sauti yako ya ndani inayokusemesha kwa
ajili ya hatima yako na mafanikio unayotaka. Kumbuka karibu asilimia 90
ya mafanikio yako yanahitaji msimamo wa kudumu unaoanzia ndani yako.
Amua kujifunza mara kwa mara mambo yanayoweza kuifanya sauti yako ya
ndani kuwa halisi kila wakati juu ya mafanikio unayotaka ili uweze
kujenga misingi chanya ya kukupeleka katika kilele cha ndoto yako.
Ukweli ni kuwa kadiri unavyolisha akili na moyo wako mambo chanya zaidi
ndivyo sauti yako ya ndani inakua halisi na kukuelekeza mahali sahihi
unapota kufika.
Tumia kelele za wengine kama nganzi ya kukupandisha kwenye
kilele chako cha mafanikio. Ila usikubali kuumia au kutokusonga mbele
kwa sababu ya mawazo au maneno mabaya wanayokuwazia watu wako wa karibu.
Jifunze kuamini mafanikio juu yako hata kama hakuna mtu anayeamini
unachokiamini kwa Sasa. Utakapoanza kuamini wewe binafsi juu kile
unachokitaka na kuchukua hatua bila kuchoka, hii itakufanya uweke
uhalisi utakaowafanya walio kuzunguka kuona matokeo ya kile ulichokuwa
ukitafuta kwa muda mfupi. Jifunze kunyamaza, ongeza hatua.
Husiwe mmojawapo wa watu wanaoishi kwa kuangalia maneno ya
watu. Amua kupiga hatua ISHINDOTOYAKO usitazame nyuma, songa mbele. Ziba
masikio yote mawili zidi ya kelele zote zinazokuzuia kuifata ndoto
yako. Narudia kukuambia ziba masikio yote mawili na amua kuishi ndoto
yako.
Post a Comment