RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein
amezipongeza juhudi zinazochukuliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika AFDB kuendelea kuiunga mkono Zanzibar
katika kuimarisha sekta za maendeleo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akizungumza na Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) Dk.Tonia
Kandiero alipofika Ikulu Mjini Unguja leo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiagana
na Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) Dk.Tonia Kandiero
alipofika Ikulu Mjini Unguja leo baada ya mazungumzo yao,[Picha na Ikulu.
21/12/2016
Dkt. Shein amesema kuwa mbali ya Benki hiyo kutoa ushirikiano wake katika kuimarisha sekta za maendeleo hapa nchini zikiwemo maji, barabara, kilimo, nishati, afya, elimu na utawala bora pia, imeweza kutoa mashirikiano katika nyanja nyengine za kijamii, kiuchumi na kimaendeleo.
Kwa upande wake Dkt. Kandiero amemuhakikishia Rais Shein
kuwa miradi yote inayosimamiwa na Benki hiyo itakamilishwa ikiwemo miradi ya
ujenzi wa barabara zikiwemo barabara ya
Mahonda -Mkokotoni yenye urefu wa km 31, Fuoni -Kombeni km 8.6, Pale-
Kiongele km 4.6 na Matemwe - Muyuni yenye urefu wa km 7.6.
Pamoja na hayo, Dk. Kandiero ambaye amefanya kazi zake
hapa Tanzania kwa takriban miaka sita, amemueleza Dkt. Shein kuwa AFDB itaimarisha
zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na
kutoa pongezi za pekee kwa Dkt. Shein na
serikali anayoiongoza kwa kusimamia vyema miradi ya maendeleo.


Post a Comment