Mashindano ya mapinduzi Cup yameanza kutimua vumbi hiyo
jana katika uwanja wa amani kwa kuzikutanisha Jang’ombe boys na Timu ya Taifa
Jang’ombe zote kutoka mtaa mmoja wa Jang’ombe hapa Zanzibar
Mchezo huo uliorindima majira ya saa 2:30 za usiku
Taifa Jang’ombe wamefanikuiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wao
wajadi Jang’ombe Boys
Goli hilo lilofungwa na mshambuliaji mwenye makeke
zaidi uwanjani Hassani Banda litawalazimu Taifa Jang’ombe kukaa kileleni mwa kundi A lenye timu kama Simba,URA,KVZ na Jang’mbe Boys hadi mchezo wa
mwengine wa kundi hilo utakaopigwa tar 1-1-2017 utakapotoa majibu ya nani
atashika usukani wa kundi hilo
Mapinduzi Cup yataendelea tena tarehe moja baada ya
hii leo kuwa mapunziko ambapo ratiba kamili ya michezo hiyo hapo chini
KUNDI B :Yanga, Azam, Zimamoto na Jamhuri.
RATIBA MAPINDUZI CUP .
30/12/2016 Taifa ya jang’ombe vs Jang’ombe boys saa 2:15 usiku.
1/1/2017 KVZ VS URA Saa 10:00 alasiri, Simba vs Taifa ya Jang’ombe saa 2:15 usiku.
2/1/2017 Azam vs Zimamoto saa 10:00 alasiri, Yanga vs Jamhuri saa 2:15 usiku.
3/1/2017 Jang’ombe boys vs URA saa 10:00 alasiri, KVZ vs Simba saa 2:15 usiku.
4/1/2017 Zimamoto vs Yanga saa 10:00 alasiri, Jamhuri vs Azam saa 2:15 usiku.
5/1/2017 KVZ vs Jang’ombe boys saa 10:00 alasiri, Simba vs URA saa 2:15 usiku.
6/1/2017 Taifa ya jang’ombe vs KVZ saa 2:15 usiku.
7/1/2017 Jamhuri vs Zimamoto saa 10:00 alasiri, Yanga vs Azam saa 2:15 usiku.
8/1/2017 Simba vs Jang’ombe boys saa 10:00 alasiri ,Taifa ya jang’ombe vs URA 2:15 usiku.
10/1/2017 Saa 10: 00 nusu fainal ya kwanza ,Saa 2:15 nusu fainal ya pili.
13/1/2017 FAINAL saa 2: 15 usiku.
Post a Comment