0
Ummy Mwalimu
Katika kuhakikisha Watanzania wanakuwa na utaratibu wa kujihusisha na mazoezi ili kupunguza hatari ya kupata magonjwa ambayo sio ya kuambuza, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa kampeni ya kuhamasisha mazoezi ya AFYA YAKO, MTAJI WAKO, FANYA MAZOEZI, LINDA AFYA YAKO itakuwa endelevu na itafanyika nchi nzima.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akifunga mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari yaliyokuwa yanalenga kutoa elimu kwa wanahabari kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Ummy MwalimuWaziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kufunga mafunzo ya siku moja kwa waNAhabari kuhusu magonjwa ambayo sio ya kuambukiza.
“Kila mwezi tutakuwa tukichagua mkoa ambao mazoezi yatakuwa yanafanyika na yatakuwa yakiongozwa na mimi, au naibu waziri au katibu mkuu naibu katibu mkuu au hata viongozi wengine na hakutakuwa na gharama maana tunajua tukianza kuweka hayo mambo kutajitokeza changamoto nyingine,” alisema Ummy.
Waziri Ummy alisema alifikia uamuzi wa kuanzisha kampeni hiyo kutokana na takwimu kuonyesha kuwepo kwa idadi kubwa ya watu ambao wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na magonjwa yasiyo ya kuambikiza na wakati ni jambo ambalo linaweza kumalizika kama wananchi watabadili mfumo wao wa maisha na kuanza kuwa wanafanya mazoezi.
Ummy MwalimuWaziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu kampeni ya kudhibiti magonjwa yasiyo ya kuambukiza ‘AFYA YAKO, MTAJI WAKO, FANYA MAZOEZI, LINDA AFYA YAKO’.
“Nina mwaka hapa wizarani wakati nimefika kipaumbele changu kilikuwa ni afya ya mama na mtoto lakini kumbe tukasahau upande mwingine, ripoti inaonyesha kati ya watu 100 ambao wanapoteza maisha, 27 wanakufa kutokana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, sasa niamua lazima tulishughulikie jambo hili,” alisema Waziri Ummy.
Pia aliwataka Watanzania wote kujitokeza Desemba, 17 katika viwanja vya Leaders Club kuanzia saa 12:30 asubuhi katika uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasiyo ya kuambukiza ambapo mgeni rasmi atakuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
dsc_1693Afisa wa kitengo cha magonjwa yasiyo ya kuambukiza kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mariam Kalomo akiwaeleza waandishi wa habari magonjwa ambayo sio ya kuambukiza.
dsc_1711Mtaalamu wa Mazoezi kutoka PAAT (Physical Activity Association of Tanzania), Waziri Ndonde akiwafundisha waandishi wa habari aina za mazoezi na jinsi yanavyofanyika.
dsc_1721Mwanahabari Majid Mjengwa akieleza jinsi ambavyo mazoezi yana umuhimu katika maisha yake ya kila siku.
dsc_1729Mratibu wa Magonjwa yasiyoambukizwa wa mkoa wa Dar es Salaam, Dkt. Digna Riwa akieleza umuhimu wa kufanya mazoezi na kula kwa kufata ushauri wa wataalamu wa afya.
dsc_1699 Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo.
dsc_1695
dsc_1700

Post a Comment

 
Top