
Majira kama haya mwaka jana, Watanzania walikuwa wakijivunia kuwashuhudia nyota wao wawili wa kimataifa Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wakicheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa vilabu, wakiwa na mabingwa wa Afrika TP-Mazembe.

Tayari Samatta ameshapaa na kutua Genk ya Ubeligji huku Ulimwengu akiwa hana timu baada ya mkataba wake na TP-Mazembe kumalizika.
Wikiendi hii michuano hiyo itaanza nchini Japan ambapo kuna kitu kipya kimeongezwa na shirikisho la soka duniani FIFA, ambapo sasa waamuzi wa Mechi hizo watapata msaada wa maamuzi yao kwa kutumia Video kutoka kwenye Mfumo wa Majaribio uitwao VARs, Video Assistant Referees.

Post a Comment