0


Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Shinyanga amewatoa hofu wananchi wa mkoa huo na kuwataka wajiandae kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka  bila wasiwasi kwakuwa jeshi la polisi mkoani humo limejipanga kukabiliana na wahalifu wanaotumia fursa ya sikukuu hizo kufanya vitendo vinavyovunja sheria.
 
ACP Muliro Jumanne Muluro ameyasema hayo wakati wa mazoezi ya utayari ya vikosi vya Jeshi la polisi mkoani Shinyanga mazoezi ambayo yanafanyika kwa kuzunguka mitaa yote ya mji na vijiji mkoani Shinyanga kwa lengo la kutambua maeneo korofi yanayotumiwa na wahalifu kujificha ambapo amewataka wakazi wa mkoa wa huo kusherehekea sikuku ya Krismasi na mwaka mpya kwa amani bila kufanya vurugu huku akitoa onyo kwa yeyote atakayesababisha au  kufanya vurugu.
Baadhi ya askari wa Jeshi la polisi mkoani shinyanga wanaoshiriki katika mazoezi ya utayari wa kupambana na wahalifu wamedai kuwa mazoezi hayo yanawajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao na hapa wanaeleza jinsi wanavyojipanga kulinda raia na mali zao katika kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka na baada ya sikukuu kumalizika.

Post a Comment

 
Top