Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini, (TANESCO), Mhandisi
Felchesmi Mramba, (katikati), akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam, leo Novemba 24, 2016. Alikuwa akitoa
ufafanuazi kuhusu masuala muhimu ya TANESCO. Wengine pichani, kulia ni
Meneja wa Vyuo vya TANESCO, Mhandisi Said Msemo na kushoto ni Kaimu
Meneja Uhisano wa Shirika hilo, Leila Muhaji.NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo
Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji, (kushoto), akizunguzma jambo
SERIKALI kupitia Shirika lake la umeme nchini TANESCO limefanya
uwekezaji mkubwa kwenye miradi mbalimbali ya umeme yenye thamani ya
Shilingi Trilioni 5.35, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Mhandisi
Felchesmi Mramba amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,
leo Novemba 24, 2016.
Akitoa ufafanuzi juu ya masuala mbalimbali muhimu ya Shirika hilo,
Mhandisi Mramba alisema, “Katika historia ya sekta ya umeme, haijawahi
kutokea uwekezaji mkubwa kufanyika kwa wakati mmoja kama ilivyo sasa,
Miradi yote ya umeme inayoendelea na ambayo tayari iemtengewa fedha ina
thamani ya Shilingi Trilioni 3.85, na majadiliano kati ya Serikali na
Exim Bank ya mradi wa Dar es Salaam-Arusha wa Shilingi Trilioni 1.5
yakiwa katika hatua za mwisho.” Alifafanua Mhandisi Mramba.
“ Uwekezaji huu unathibitisha kwamba nia ya Serikali ya awamau ya tano
ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda sio ya maneno matupu bali
inaambatana na vitendo kwa uwekezaji madhubuti kwenye umeme.” Alisema.
Mhandisi Mramba alitaja Miradi hiyo mikubwa ya umeme kuwa ni pamoja na
ule wa upanuzi wa Kinyerezi I, Kinyerezi II, mradi wa Backbone,
Kenya-Tanzania, TEDAP, Makambako-Songea, Uboreshaji umeme jijini Dar es
Salaam, City Centre-Dar es Salaam, Electricity V, Bulyanhulu-Geita,
Geita Nyakanazi na Rusumo Power Plant (T), miradi yote hii ikiwa na
jumla ya thamani ya Shilingi Trilioni 3.85.
Post a Comment