0

Nini unachoweza kufikiri kwa mara ya kwanza pale unapoambiwa kukubali kudharaulika kunaweza kukuongezea nguvu ya kufanikiwa kule unapoelekea, tofauti kabisa na ulivyowahi kufikiri hapo kabla? Ni rahisi kunifikiria vibaya na kusema nimechanganyikiwa. Yawezekana kwa namna yoyote utakavyofikiri, lakini Je, hizi ni fikra sahihi kwangu? Ukweli ni kwamba kama unajihisi unapitia mahali pa kudharaulika kwenye eneo fulani katika maisha yako, basi una nafasi kubwa ya kuweza kufanikiwa kama utasimama imara katika nafasi yako sahihi pasipo kuteteleka.

Wakati watu wengine wanatumia muda mrefu kukudhoofisha na kukufanya uonekane mnyonge katika maisha yako, hasa kwa sababu ya kuangalia hali yako na mahali ulipotoka kifamilia, kiwango chako cha elimu pamoja na kiwango chako cha kiuchumi; haupaswi kuzingatia kila jambo wanalokusema na kukunyoshea kidole bali amini katika uwezo mkubwa ulionao ndani yako. Fahamu kudharaulika kwako kunakuandaa katika nafasi ya juu (greatness) ya mafanikio yako.
Hapa chini nimekupatia sababu 3 kwa nini kujishusha na kuonekana mdogo kunaweza kukupa nafasi ya kuwa mshindi:

1: Historia inathibitisha jambo hili. Watu waliodharaulika ndio waliotawala.
Kutokea kipindi cha Daudi na Goliathi hadi Donald Trump, historia inatuonyesha kwamba kukubali kudharaulika na kuonekana hufai kwa kipindi fulani, hiyo ndio imekuwa ni silaha na siri kubwa ya mafanikio na ushindi wa watu wengi duniani. Katika historia ya kweli inayomuhusu Daudi na Goliathi, utaona Daudi pamoja na udogo wake aliokuwa nao hata kufikia kudharaulika na jitu kubwa lenye uwezo alilokuwa akipambana nalo; hii haikumfanya Daudi kuangalia majigambo na dharau za Goliathi na watu wake wa karibu bali aliamua kupambana hadi alipopata ushindi. Kejeli za maadui zake hazikumpunguzia ari yake (moral) ya kutafuta kushinda sawa na picha ya halisi aliokuwa amebeba ndani yake.

Ilikuwa si rahisi sana kwa watu wa upande wa Goliathi na hata baadhi ya ndugu zake na Daudi, kuamini kuwa Daudi anaweza kushinda vita ile na kufikia kumwua na kumwangamiza Goliathi kwa haraka. Na hiki ndio tunachokiona kwa mshindi wa uraisi katika taifa la Marekani Donald Trump. Pamoja na kusemwa sana na hata kudharaulika na watu wengi kwamba hatofanikiwa kushinda na kushika nafasi ya uraisi, Donald Trump ameithibitishia dunia yote baada ya kuwa imara na hata kuwa mshindi wa kinyanganyiro hicho cha uraisi katika taifa kubwa duniani. Unahitaji kutokukata tamaa hata kama watu wote hawataamini uwezo mkubwa ulionao ndani yako, amua kuamini ndoto yako hadi utakapoona ushindi ukitokea mbele yako. Jifunze kwa Daudi na Trump na watu wengine waliofanikiwa kisha amua kuchukua hatua juu ya ndoto yako.

“When I write, I try to represent the voices of people I’ve known who had no voice.”
―Carla H. Krueger
2: Unapoonekana hufai ndio wanakuongezea umakini (focus) na kujifunza zaidi.
Siku moja wakati naangalia filamu ya Jaden Smith ambaye ni mtoto wa mwigizaji maarufu wa Marekani Will Smith aliyoicheza yeye (Jaden Smith) pamoja na Jackie Chan, filamu inaitwa The Karate Kid Drama, kuna kitu kikubwa sana kinachohusu mafanikio nilichojifunza ndani ya filamu hiyo ambayo ni ngumu kuisahau. Baada ya Jaden Smith kuonekana hafai na tena ni mdhaifu katikati ya adui zake ambao ni watoto wenye asili ya kichina, hata ikafikia kuwahofia kila anapokutana nao kwa sababu ya uwezo na nguvu walizokuwanazo katika kupigana karate. Hii ilimfanya Jaden kuwa mnyonge na hata kuamua kutafuta shule na mwalimu mzuri wa kumfunza namna ya kupigana na kuwa imara katika mchezo wa karate. Ukweli ni kwamba baada ya Jaden kuamua kurudi upya na kukaa chini ya mwalimu wake Jackie Chan na kufundishwa namna kamili ya kupigana, alijikuta anafanikiwa kuwashinda adui zake wote katika mechi ya mwisho aliyoicheza.

Jambo hili ni wazi na halisi katika maisha yetu ya kila siku hapa duniani. Haupaswi kukata tamaa na kuangalia ni wapi umeshindwa au kudharaulika, bali unachotakiwa ni kuangalia ndoto yako na ushindi unaoutaka katika maisha yako. Hata kama watu wakikudharau na kukucheka leo kutokana na kiwango chako kidogo cha upeo ulichonacho, mwamini Mungu na amini katika uwezo wako aliokupa, amua kujifunza na kutafuta kujua namna ya kuweza kufanikiwa na kuelekea katika kilele cha mafanikio yako.

3: Watu wanaoanzia chini ni ngumu kupoteza mafanikio yao.
Kama utaamua kuanzia chini au hapo ulipo, hautokuwa na chochote cha kupoteza kwa hapo badae. Wakati unaonekana ni mtu wa hali ya chini au haufai kwa watu waliokuzunguka, basi ni vizuri kuamini katika uwezo wako na kuamua kuangalia ni wapi unapotaka kufika, hii ni moja ya njia nzuri ya kuweza kukusaidia kutimiza malengo na ndoto zako kwa haraka zaidi. Mara nyingi watu wengi inapotokea wanasemwa kidogo tu na watu wa karibu yao, huwa wanafikia kukata tamaa hata kushindwa kuendelea mbele dhidi ya kutafuta ushindi wanaoutarajia. Kujishusha na kuamua kudharaulika eneo fulani kwa kipindi kifupi, nafasi hii itakupa nguvu na uwezo wa kujifunza mambo mengi zaidi, ambayo kwa hayo utakuwa umeamua kujijengea ndani yako misuli ya imani na mafanikio dhidi ya kule unapoelekea.

“Look for the person everyone hates, and love them.”
―Criss Jami
Hauhitaji kusubiri watu wakuthibitishie uwezo wako mkubwa ulionao ndani yako, kisha uanze kuchukua hatua dhidi ya ndoto yako. Hauhitaji kumwomba mtu yoyote ruksa ya kutimiza maono na picha uliyonayo ndani yako; unahitaji kuweka malengo na vipaumbele vyako muhimu ili uweze kuchukua hatua kila siku katika kuhakikisha unafanikiwa. Kwa mfano, kama unafanya biashara yenye kipato cha hali ya chini na unatamani kufanikiwa na kufungua biashara nyingine, amini unaweza kufanya hivyo kama utaamua kujiamini na kujikubali kuwa unaweza.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top