0


Waziri wa Elimu, Profesa Joyce  Ndalichako.
Serikali imebaini kuwepo kwa vyuo vikuu vingi visivyo na sifa, hivyo inakusudia kuvifuta lengo likiwa ni kuhakikisha inaimarisha kiwango cha elimu inayotolewa kwa ngazi zote.  

Waziri wa Elimu, Profesa Joyce  Ndalichako ameyasema hayo  leo (Jumatatu), wakati akifungua  mkutano wa siku mbili wa  wadau wa elimu ya juu.
Amesema hayo yamebainika baada ya jopo la wataalamu kufanya uhakiki kwenye vyuo hivyo nchini.
“Lengo ni kuhakikisha wasomi wanaohitimu kwenye vyuo hivyo wanakuwa wameiva kitaaluma, ili pia waweze kushiriki katika kuijenga Tanzania ya viwanda,” amesema  Profesa Ndalichako.
Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya vyuo vikuu nchini(TCU) Profesa Jacob Mtabaji amesema  wamejipanga kuhakikisha kwamba wanafanyakazi zao kwa kusimamia mwongozo uliopo ili kuondoa uwepo wa vyuo vingi visivyo na sifa.

Post a Comment

 
Top