Arsenal
wanakabiliwa na kibarua kumaliza wakiwa wanaongoza kwenye kundi lao
mechi za Kombe la Klabu Bingwa Ulaya baada ya kutoka sare na Paris
St-Germain (PSG) katika uwanja wa Emirates Jumatano usiku.
Gunners
walitaka ushindi ili kuwawezesha kuwa kileleni katika kundi A baada ya
miaka mingi kumaliza wa pili na kuondolewa mara sita katika timu 16 bora
katika hatua ya muondoano.
Edinson Cavani alipata bao la kwanza katika dakika ya 18.
Olivier
Giroud, alifunga penalti kabla ya mapumziko baada ya Grzegorz
Krychowiak kusababisha ikabu kwa kumchezea visivyo mshambuliaji Alexis
Sanchez. Marco Verratti alifunga bao la pili katika dakika 60.
PSG pia walikuwa hatari huku Lucas akipiga mpira wa kichwa uliomgusa Alex Iwobi na kuwawezesha kusawazisha katika dakika ya 77.
Cavani alikosa nafasi mbili nzuri za kufunga.
Ingawa
Arsenal na PSG wana alama sawa kila mmoja akiwa amesalia na mechi moja,
mabingwa hao wa Ufaransa wana nafasi bora kwa kuzingatia matokeo baina
ya klabu hizo mbili.
PSG walifunga mabao mengi ugenini, Emirates
kwenye sare hiyo ya Jumatano. Klabu hizo zilipokutana Paris, zilitoka
sare ya 1-1, hivyo Arsenal wana bao moja pekee la ugenini mechi baina ya
klabu hizo.
Kukosa kwa Arsenal kuongoza hatua ya makundi
kumewasababishia kupangwa na klabu hatari, zinazoongoza makundi, na
hivyo kushindwa kupita hatua ya 16 bora kwa miaka 7.
PSG
watakutana na Ludogorets katika mechi yao ya mwisho, timu ambayo Arsenal
iliichapa mabao 6-0 , huku Wenger na vijana wake wakielekea Basel.
Post a Comment