0


tarimepic
Kikosi kazi cha ukaguzi wa miondombinu ya shirika la umeme (TANESCO) kinachozunguka nchi nzima kusaka wateja wakubwa wanaoiba umeme kimebaini shirika kupoteza zaidi ya sh Bilioni 1 na milioni 300 katika mikoa 19 waliyotembelea.
 
Kikosi hicho kinachoongozwa na  na Bw John Manyama wakiwa mkoani Kagera, wamebaini wizi wa umeme wa zaidi ya milioni 400 katika mkoa huo pekee, na hiki ni kiwanda cha kusaga na kukoboa nafaka kilichoko Muleba Mkoani Kagera, ambacho inaelezwa kuwa wamekuwa wakitumia umeme bila kulipa kwa kipindi cha miaka 2 hivyo kiwanda hiki pekee kusababisha hasara ya milioni 300.
Bw John Manyama akiongea  na waandishi wa habari katika kiwanda hicho amesema  Umeme katika kiwanda hicho umekatwa, na mmiliki anahesabika kama mwizi wa umeme.
Hata hivyo uongozi wa kiwanda hicho haukupatikana baada ya mmiliki kudaiwa kuishi Jijini Dar Es salaam, huku anayedaiwa mkewe kugoma kuongea na  baadhi ya vibarua waliokutwa katika kiwanda hicho wakionekana kutoelewa chochote, na kuomba kifunguliwe ili waendelee na kazi.
Imeelezwa kuwa ukaguzi katika mikoa mingine unaendelea, na kwamba wote waliobanika kuiba umeme wanapewa mwezi mmoja kulipia bila faini,kwamba  baada ya mwezi mmoja  bila kulipa watafikishwa mahakamani.

Post a Comment

 
Top