0

Baadhi ya wakandarasi wanaotekeleza miradi ya barabara mkoani Arusha wameshindwa kuendelea na kazi kutokana na ukosefu wa maji kulikosababishwa na kukauka kwa vyanzo vya maji.
Wakiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi kwenye kikao cha bodi ya barabara  mkoa wahandisi wa wilaya zinazokabiliwa na tatizo hilo ikiwemo ya Ngorongoro wamesema tatizo hilo ni kubwa na kazi zote zinazohitaji maji katika miradi hiyo zimesimama hadi hapo mvua zitakaponyesha kwani kiasi cha maji kinachopatikana hakiwezi kukidhi mahitaji. 
Katika hatua nyingine mhandisi wa mkoa bw,edwaerd amboka amesema pia katika  kufuatilia utekelezaji wa miradi ya barabara wamebaini kuwepo kwa wakandarasi  wamebainika kuwepo kwa baadhi ya wakandarasi wasio na uwezo na waliopata tenda kwa  udanganyifu na huku Katibu Tawala anayeshughulikia miundombinu naye akielezea  uwepo wa tatizo la matumizi mabaya ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya miundombinu.
Akizungumzia tatizo la kusua sua kwa miradi na mingine kusimama kutokana na tatizo  la maji mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni Mkuu wa mkoa wa Arusha Bw Mrisho  Gambo amesema zipo taratibu za kufuata zinazpojitokeza changamoto kama hizo na  kuhusu wakandarasi walioidanganya serikali ameviagiza vyombo vinavyohusika ikiwemo TAKUKURU kuhakikisha sheria inachukua nafasi yake kwa wote walioshiriki  kufanikisha  udanganyifu huo. 
Arusha ni miongoni mwa mikoa inayokabiliwa na tishio kubwa la ukame linalohusishwa  na mabadiliko ya tabia ya nchi,ukame na uharibifu wa mazingira ambao umesababisha asilimia kubwa ya vyanzo vya maji kukauka,na kwa sasa  asilimia kubwa ya wananchi wanategemea maji visima ambavyo hata hivyo bado ni upatikanaji wake ni mgumu.

Post a Comment

 
Top