0


Utafiti uliofanyika nchini marekani umebaini kwa kila ndoa mia moja  zinazofungwa, hamsini zinavunjika..hali hii pia hapa africa ni mbaya sana japokua hakuna tafiti zilizofanyika kuangalia hali halisi ikoje. kumekua kuna makosa mengi sana yanafanyika kabla ya kuoa au kuolewa, yaani watu hufikiria sana jinsi gani watakua na furaha siku ya harusi bila kufikiria itakuaje baada ya harusi.

Watu hawaangalii hali halisi ikoje na kupofushwa na yale mapenzi motomoto bila kujua kwamba ni ya muda tu  na ipo siku mapenzi  yatapoa na macho yako yatafunguka kuona ukweli.kikristo ndoa ni pingu ya watu wawili ambayo ukiingia hutakiwi kutoka huko mpaka kifo chako hata kwa waislam na imani zingine ambazo zinaruhusu mke zaidi ya mmoja usipokua makini wake zako wote wanne watakushinda.ndoa ina changmoto nyingi sana lakini baadhi ya changamoto watu huziona kabla ya ndoa na kuingia nazo kwenye ndoa bila kujua huo ndio utakua msiba wa maisha yao.yafuatayo ni mambo ya msingi sana yakuzingatia kabla ya kuingia huko.

1. Mapenzi iwe sababu kuu ya ndoa; kuna watu wengi sana wameingia kwenye ndoa bila kuzingatia hili... watu wameingia sababu ya kufuata mali[hasa wanawake], sababu ya presha za familia zao, sababu ya upweke, sababu ya kuona umri umeenda sana, sababu ya kuridhisha watu fulani, sababu kwamba na wao waonekane wameoa au kuolewa, kwasababu alizaa na muhusika na kadhalika ....kumbuka kama unayemuoa au kuolewa nafsi yako haijaridhika naye utaishi kwa mateso maisha yako yote.hutaweza kushiriki tendo la ndoa kwa amani na wala hutaweza kuonyesha mapenzi kwa aina yeyote ile hata ukijalizimisha utashtukiwa tu.

2. Zingatia swala la imani za kidini; swala hili unaweza kuliona dogo kabla ya ndoa au ukaliona kubwa lakini ukalifumbia macho kwasababu umependa lakini kumbuka ndoa haziunganishi watu wawili tu, ndoa huunganisha familia mbili.utafiti umeonyesha kutoelewana kabisa kwa familia za imani tofauti zikikutanishwa na ndoa.mfano mkristo kumuoa muislam. kama unaona familia ya muhusika haijaridhika na iko tayari kukutenga au kumtenga mwenzako basi achana na hiyo ndoa kwani itakupa msongo wa mawazo maisha yako yote na siku watoto wakizaliwa ugomvi ndio utakua mkali zaidi kwani kila familia itataka mtoto afuate imani yao.kuepusha hili tafuta mwenye imani kama yako au upate baraka za familia zote kabla ya ndoa na muelewane kuhusu imani za watoto.kumbuka familia bora ni ile inayosali kwa pamoja.

3. Zingatia swala la ugomvi; kama mtarajiwa wako ameshaanza kukupiga makofi sasa hivi basi ujue baada ya ndoa itakua mapanga na rungu. mtu alizeyezoea kupiga hataacha kukupiga kamwe hata akisema atabadilia usimsikilize kwani muda wa kubadilika ni kabla ya ndoa.kuna watu wengi sana wameuawa sababu ya vipigo ndani ya ndoa.

4. Zingatia swala la heshima; hii ni muhimu sana hasa kwa wanaume... wewe ndio unaenda kua baba wa familia hivyo kimsingi kauli ya mwisho inatakiwa itoke kwako. usioe mwanamke ambaye huwezi kumkemea kufanya kitu fulani kwani ataitesa nafsi yako mpaka utakapokufa.kama huwezi kumwambia usifanye hiki akakusikiliza basi huyo hakufai.

5. Zingatia swala la uchumi; uko tayari kuhudumia familia kwa uchumi wako? utakayefunga nae ndoa ndiye atakaye amua kama mtakua matajiri au masikini. je unaweza kumiliki mtu ambaye hawezi kujishughulisha kwa lolote? swala la kusoma au kua na kazi sio muhimu sana kwani kuna mfano wa watu wengi ambao sio wasomi lakini wana maisha mazuri na kama kasoma hana kazi huenda atapata siku moja.kama mwenzio haonyeshi dalili ya kujituma kutafuta pesa, sio mchumi yaani kila siku mnalazimika kula hotelini na wakati jiko mnalo, ana imani wewe ndio kila kitu basi kimbia mbali. hali ya dunia kiuchumi ni mbaya sana kuna uwezekano hata ukiugua muda mrefu au ukifa watoto watakufa na njaa kwani mwenzio anakutegemea wewe.tafuta muhangaikaji kama wewe au angalau jaribu kumbadilisha kama akibadilika sawa.

6. Zingatia swala la watoto wa nje; lazima iwekwe wazi watoto waliozaliwa nje wataishi vipi kama familia.swala hili ni changamoto sana hasa kwa mwanaume mwenye watoto, mara nyingi wanaume hua hawajali sana kuishi watoto ambao sio wao lakini wanawake wanaweza kuwapa hata sumu watoto wa mume.kama huwezi kuvumilia na kuhudumia watoto ambao sio wako basi achana na hiyo ndoa.uliyezaa nae ni kikwazo kikubwa sana kwa mwenza wako wa sasa. kaa mbali na huduma zake zote za kifedha au mawasiliano naye yeyote. anaweza kua na haki ya kuona mtoto, ni vizuri ukampa ratiba za shule awe anenda kumuona huko lakini walimu wasimruhusu kuondoka naye.lakini kikubwa ni kwamba kama huna moyo wa chuma basi usijaribu ndoa hii.

7. Zingatia swala la magonjwa ya kurithi; kama familia zenu zina magonjwa yanayofanana na ya kurithi mfano albino, siko seli, kifafa, magonjwa ya akili, na kadhalika basi nendeni mkapime kujua kama kuna uwezekano wa nyinyi kuzaa watoto wa aina hiyo.japokua baadhi ya vipimo hapa kwetu havipo.ikithibitika kuna uwezekano wa kuwazaa basi achana na hiyo ndoa usije kuleta viumbe duniani ambavyo vitateseka sana na wewe utateseka sana kuwahudumia.

8. Zingatia mahusiano yaliyopita; ni vizuri kujua mahusiano yaliyopita yaliisha vipi yaani watu waliachana kweli au kuna sababu ambazo ziko nje ya uwezo wao ziliwafanya waachane lakini bado wanapendana.mfano umbali kutoka kwa mpenzi wa zamani, yeye aliachwa lakini bado anampenda, mpenzi kutokua tayari kuoa au kuolewa kwasababu za kiuchumi au sababu zake binafsi au familia kumkataa.fuatilia kama kama wana mawasiliano na uhakikishe mapenzi yaliisha na wewe ndio unayependwa kwa sasa lakini bila hivyo utaendela kusaidiwa na kuna mifano hai mpaka leo yaani vikao vya harusi vinaendelea lakini mtu bado anatembea na mtu wake wa zamani.

9. Zingatia tabia za mwenza wako; binadamu tuna tabia mbalimbali na kila mtu kuna jinsi anazitafsiri tabia hizo kwa upande wake mwenyewe.kama kuna tabia yeyote ambayo binafsi huipendi kwa mwenza wako mfano ulevi, umalaya, hapendi, hajui na hataki kupika, kwenda disco, kuvaa nguo za ajabu, uchafu,kutokwenda kuabudu, matusi, hasira za ajabu, na ameshindwa kuiacha tabia hiyo kabla ya ndoa basi achana nae na sio kwamba hataolewa au kuoa lakini waaachie watu wanaoweza kumvumilia.wewe unaweza kua hupendi kitu hiki ila mwingine haoni kama ni tatizo.

10. Kua mvumilivu; hili ndio swala kubwa ambalo linafanya ndoa za wazee wetu ziweze kudumu mpaka leo, kama wewe unaona kuna matatizo yatakuja ukiingia kwenye ndoa au tayari umeshaingia huko na umejikuta tayari umekabwa silaha ya uvumilivu ndio ambayo unatakiwa uwe nayo sasa hivi. hata kama ukiingia kwenye ndoa na mtu ambaye hana dosari yeyote lakini kuna changamoto za hapa na pale lazima zitatokea na inabidi uzivumilie.

Mwisho; mambo niliyotaja hapo juu kuna uwezekano unayaona kwenye nahusiano yako tayari lakini unashindwa kufanya maamuzi magumu sababu una mapenzi makubwa juu ya huyo mwanaume au mwanamke. muda kwa kufanya maamuzi ni sasa kama huamini waulize walioingia tayari na sasa wanajuta.

Post a Comment

 
Top