0


Mapenzi ni kitu kitamu sana hapa duniani na hata hupelekea mambo mengine yasiyohusiana na mapenzi moja kwa moja kuwa kwenye mstari nyoofu iwapo tu utakuwa unapendwa na kupenda pia.

Na mapenzi ni kitu kibaya sana kama utafanya kinyume na itarajiwavyo kwenye mahusiano na huweza hata kusababisha mambo mengine yasiyohusiana na mapenzi kwenda mrama/kombo.

Yafuatayo ni baadhi ya makosa ambayo unaweza kuyafanya ukidhani ni madogo sana lakini kwa wengi hupelekea mahusiano kuvunjika mara moja na kubaki unajuta na kulaumu kwa kile ulichofanya na ambacho ungeweza kukizuia wewe mwenyewe;

PUNGUZA KUJALI
Hakuna kitu kinachovunja mapenzi kirahisi kama iwapo tu ulikuwa unajali sana mwanzo wa mapenzi yenu lakini ghafla ukapunguza kumjali mwenza wako na kuanza kufanya vitu tofauti na matarajio yake.
Hakuna kitu kizuri kwenye mapenzi kama careness kwa mpenzi wako, hurefusha mapenzi sana na tofauti na hapo mapenzi huvunjika.

KUWA MLALAMISHI
Hii ni kitu nyingine kibaya sana kwenye mahusiano, hakuna mtu anayependwa kusikia mwenza wake analalamika tu kila siku. Ukiwa ni mtu wa kupenda kulalamika sana kwenye mahusiano basi kuna hatari sana ya kuja kukimbiwa mbeleni na umpendaye siku akichoka hiyo tabia.

ACHA WIVU
Kuna msemo unasema ‘’hakuna mapenzi bila wivu’’. Hii inaweza kuwa kweli kwa namna moja ama nyingine. Ulishazoea kuonyesha wivu kwa mpenzi wako lakini ghafla siku hizi unachukulia poa kila kitu na hata huna wivu hata afanye kitu ambacho ungeonyesha wivu, hapo lazima kutakuwa na ‘’doubt’’ na itapelekea kuchunguzwa na mwenza wako na mwishowe atagundua vitu vitakavyopelekea uhusiano kufa.

KUWA BIZE
Hiki ni kitu hatari sana kwenye mapenzi na huwatokea wengi sana hasa wale wafanyakazi na wafanyabiashara wakubwa, wapo bussy sana kiasi kwamba wanakosa hata muda wa kukaa na wenzi wao na kufahamu mengi kuhusu uhusiano wao.

SALITI
Hiki ni mojawapo ya vigezo hatari sana kwenye mahusiano ambavyo husababisha wengi kuachana na kuanza maisha mapya ya kimapenzi bila wawapendao kuwepo, mwenza wako akigundua kuwa umem-cheat huumia sana na ni wachache sana huweza kuvumilia na kusamehe lakini wengi huchukua maamuzi ya kuondoka.

KOSA MSIMAMO
Hii pia husababisha wenza wengi kukimbia iwapo tu uliyenaye kwenye mahusiano ataonyesha kuanza kukosa msimamo kwenye mapenzi yenu. Hii hali huogopesha wengi na kuamua kukimbia na kuanza maisha mapya kimapenzi na mwingine tofauti na wewe.

KUTOKUWA NA MALENGO
Hakuna mtu wa dunia ya sasa anayependa awe na mtu asiye na future ya maisha yake binafsi wala ya maisha yao kama wapenzi. Si msichana wala mvulana, wote siku hizi kabla ya kuwa na wewe huangalia kwanza kama wataweza kuishi na wewe na je una akili yoyote ya kufikiria maisha ya baadae au umejisahau unawaza starehe tu bila kujua kesho itakuwaje.

Post a Comment

 
Top