0



Waziri wa  mambo ya  ndani Mwigulu Mchemba amevitaka Vyombo  vya ulinzi  na usalama  mkoani Lindi na Mtwara   kuimarisha  ulinzi kwenye maeneo ya  bahari  na  kuwatega   kuwakamata watu wote  wanaotumia bandari bubu  kupitishia   magendo   pamoja  na  madawa ya kulevya
Agizo hilo amelitoa  wakati alipokuwa anazungumza  na  vikosi  vya ulinzi na  usalama  mkoani hapa  kwenye ziara yake ya kikazi ya  siku  moja
Mchemba alisema kuwa mkoa wa Lindi una changamoto  nyingi ikiwemo  bandari bubu na uwepo wa hali hiyo ume sababisha upitishaji wa madawa ya kulevya na  bidhaa  za magendo na kupelekea  kukwepa kodi
Alisema  niwajibu wa vyombo vya ulinzi  kuhakikisha  vinapamnana na wanakamatwa  watu wote  wanaojiusisha  na shughuli hiyo pia  zoezi hilo linatakiwa kuwa endelevu kwa  hatima ya  vijana na  maslai  pana ya taifa.
Mchemba aliongeza kwa kusema  suala la  ulinzi na  usalama  halina mjadala  hivyo kila  mtanzania  anawajibu wa  kulinda amani  na mtu yoyote atakaye  diriki kuchezea amani ya   nchi  hatakuwa  ni adui wa wa wote   hataweza kuvumiliwa
Awali akitoa taarifa  mwenyekiti wa  kamati ya ulinzi na  usalama ya   mkoa mkuu wa  mkoa  wa Lindi  Godfrey Zambi  alisema mkoa  wa Lindi  unachangamoto nyingi  za  kiulinzi  ikiwemo  kuwepo kwa wakimbizi 1892  waliotoka  nchi  Msumbuji  ambao urai  wao  hawatambuliki hadi sasa.
Zambi alimuomba  wa Waziri  huyo  wa  mambo ya ndani  kuwatambua  wakimbizi hao kwa kuwapa uraia wa kudumu  kama  watanzania au kuwarudisha  kwao ili wakaendeleze  nchi yao.
VIKOSI VYA ULINZI  NA USALAMA  MKOANI LINDI VIKIMSIKILIZA WAZIRI WA MAMBO YA  NDANI  MWIGULU  MCHEMBA

Post a Comment

 
Top