0



Naibu  waziri wa  Maliasili na  Utalii Injinia Ramo  Makani   amesema wizara  imejipanga kuboresha  na kuimarisha vivutio vya  vya utalii  wa ndani  ikiwemo   Mali kale na  fukwe za  bahari na hoteli za  kitalii ili kuongeza pato la taifa
Hayo  aliyasema juzi wakati alipokuwa  anazungumza  na  wa wananchi wa  vijiji vya Mtoni  wilaya  Kilwa na Kijiweni wilaya  ya Lindi  kwenye ziara  yake ya  kikazi ya siku  moja  mkoani Lindi
Makini Alisema ili  kutumia vizuri fursa za maliasili zilizopo nchini  katika kukuza uchumi wa taifa serikali  haina budi  kuboresha huduma hizo ili iweze kuleta tija kwa  kuchangia pato la taifa na kukuza  uchumi wa nchi yetu
“ipo sababu ya  kuongeza nguvu katika  sekta ya  utalii  na maliasili  ili iwe  miongoni mwa sekta zinazotumainiwa nchini kwa  kuongeza  pato la taifa  hatimaye kukuza uchumi wa Taifa “ alisema  Makani.
alisema kuwa Wizara inalengo la  kuboresha miundombinu ya vivutio vya ndani na kulinda na kuhifadhi  na mazingira ili, kuboresha utoaji wahuduma pamoja na kuendeleza vivutio vilivyopo na kuanzisha vivutio vipya.
Injinia  Makani alisema utalii wa  ndani ukiimarishwa  utaweza kuongeza  mapato ambayo  yataweza kuwa  sawa  na  mapato yanayotokana  na  watalii wa nje kwani  jamii kwa sasa  ina mwamko mkubwa wa kutembelea vivutio vilivyopo hapa nchini.
Aidha  naibu  waziri  amewataka wananchi  wanaoishindi  kando kando ya ufukwe  wa bahari  hindi kutorubuniwa  na  matajiri  na kuanza  kuuza   maeneo yao ovyo  badala yake kuendelea  kuulinda
Kwa  upande wa Mkurugenzi mtendaji  wa halmashauri ya wilaya Kilwa  Zablon Bugingo  alisema  kuwa halmashauri ya  wilaya  Kilwa imeanza  mikakati ya kuboresha  kwa  kufanya ukarabati Magofu  ya  zamani  kwa kushirikiana  na wadau mbalimbali ili  yaweze kuingiza  mapato




Post a Comment

 
Top