0

Dodoma.Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imebaini madudu ndani ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambayo yalitafuna fedha kibao za walipakodi.

Fedha hizo zilitumika katika kuandaa bila mafanikio tamasha la kuchangia mradi mmoja ambalo lingefanyika nchini Marekani, wakati fedha za ujenzi wa ofisi za makao makuu ya wizara hiyo zililipwa kwa mkandarasi kabla ya mkataba kusainiwa na hadi sasa halijajengwa.

Mbunge wa Bagamoyo, Shukuru Kawambwa alilazimika kutoa majibu mbele ya kamati hiyo kwa kuwa wakati huo alikuwa Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Post a Comment

 
Top