Korea Kaskazini imelitaka kundi la wafanyikazi wa mkahawa mmoja waliohamia nchini Korea Kusini mapema mwezi huu kurudi nyumbani.
Wito huo ni hatua ya kwanza ya taifa hilo kufuatia tangazo la maafisa wa Korea Kusini kwamba kundi hilo limeachiliwa huru.
Wafanyikazi
hao waliamua kuhamia nchini Korea Kusini mnamo mwezi Aprili kutoka
mkahawa mmoja wa Korea Kaskazini katika mji wa kichina wa Ningbo.
Korea
Kaskazini inasisitiza kuwa kundi hilo lilitekwa nyara na huduma ya
kitaifa ya ujasusi ya Korea Kusini,lakini Korea Kusini inakana hilo
ikisema raia hao walihama kwa kupenda kwao.
Post a Comment