
Unajua katiba? Ni muundo wa sheria, kanuni zinazoainisha jinsi ambavyo nchi, chama au shirika vitakavyoendesha shughuli zao.
Uhusiano wa kimapenzi upo katika mtindo wa kitaasisi lakini kwa
bahati mbaya katiba yake haipo kwenye maandishi (non-written constitution).
Uhusiano wa kimapenzi upo katika mtindo wa kitaasisi lakini kwa
bahati mbaya katiba yake haipo kwenye maandishi (non-written constitution).
Makala haya yataiweka katiba hiyo kwenye maandishi kwa ajili ya kukusaidia msomaji wangu kujua jinsi ya kuishi ndani ya uhusiano wako.
Wengi wamekuwa wakipata tabu, wanapotoka na kuishi nje ya mistari inayofaa kwa sababu hawajaisoma au hawaijui.
Unahitaji muongozo wa kikatiba ili mapenzi yako yasitawaliwe na migogoro. Unatakiwa ujue jinsi ya kuishi kwa upendo na furaha.
Amani itawale kwenye uhusiano, hali kadhalika tabia zako zikidhi
mahitaji ya katiba ya mapenzi au ndoa yako.
Je, unatakiwa uyafanyie nini mapenzi yako au ndoa yako? Muonekano wako uweje mbele ya mwenzi wako?
Ukiwa
na hasira, ni kitu gani cha kufanya? Inapotokea mpenzi wako
ameghadhabika, jambo lipi ufanye liweze kumrudisha kwenye mstari
unaotakiwa?
Ndoa
inahitaji nini? Kwa nini aliye kwenye ndoa hatakiwi kujiona ana uhuru
wa kupitiliza kiasi cha kumuathiri mwenzi wake? Nini wajibu na haki za
mtu kwenye mapenzi? Ni kwa namna gani mtindo wa
maisha wa bachela, ukitekelezwa na mwanandoa ni sumu?
Hayo na mengine mengi, yanachambuliwa kinagaubaga kwenye katiba ya mapenzi.
Mtu sahihi ni yule anayeishi kwa kujiamini, si ambaye anafanya kwa kujaribu, akisubiria matokeo au mapokeo ya mpenzi
wake.
Mapenzi ni rahisi mno endapo utaheshimu muongozo.
Katiba yenyewe inaundwa na vipengele vingi ambavyo nitavichambua katika wigo mpana ili uweze kuelewa ipasavyo.
Inahitaji utulivu na umakini wakati wa kusoma, mwisho utakuwa ni mwenye
mafanikio makubwa endapo yaliyomo kwenye maandishi yangu yatakita vilivyo ndani ya ubongo.
UPENDO
Hiki ni kipengele kikuu.
Unaweza kukiita kifungu mama ndani ya katiba ya mapenzi. Huwezi kusema
upo kwenye uhusiano makini kama upendo haupo katikati. Chukua hatua madhubuti endapo utabaini upendo haupo.
Mkatae mwenzi ambaye hakupendi, kinyume chake atakupa mateso mbele ya safari.
Muongozo wa kipengele cha upendo ni kwamba lazima wewe mwenyewe uanze kuwekeza upendo kisha naye akupende.
Ni
maisha ya ubinafsi kutaraji kupendwa, wakati wewe mwenyewe huoneshi kwa
mwenzako. Zingatia hili kila siku na wakati wote ili uweze kufaidi
matunda mema kwenye uhusiano wako.
Kuna tabaka la watu ambao huishi kwa kusikilizia zaidi.
Haitakiwi kutegea, upendo unamaanisha pande mbili zinazovutana.
Huyu
anatekeleza hili kwa ajili ya mwenzake, hali kadhalika na mwingine
anasimama imara kuhakikisha mpenzi wake anafaidi malisho mema
ya mapenzi.
Hakikisha mpenzi wako hakushindi upendo, onesha unampenda zaidi.
Upendo huyeyusha mengi. Ukiwekeza upendo kwa mwenzi wako, utamfanya nafsi yake iwe na woga.
Ni rahisi kushinda vishawishi, kama atakuwa akikaa peke yake anakuwa anajiridhisha kuwa unampenda kwa
moyo wako wote.
Vinginevyo, anaweza kushawishika na kukusaliti kama tu akili yake itamtuma kuamini kwamba humpendi.
Hivyo basi, hakikisha upendo wako si wa wasiwasi. Mfanye awe na imani, ikibidi imani ya kupitiliza.
Utafiti
unaonesha kuwa mtu aliyeonesha upendo mkubwa kisha akasaliti kwa tamaa
zake, anapobainika na kuachwa hujuta zaidi kuliko yule aliyeona hakukuwa
na upendo kwa sababu haoni cha kupoteza.
Chukua
hatua madhubuti endapo utabaini upendo haupo. Mkatae mwenzi ambaye
hakupendi, kinyume chake atakupa mateso mbele ya safari.
Kuna faida kubwa mbele ya safari endapo utamkataa asiyekupenda au usiyempenda leo, kuliko kumng’ang’ania, kwani itakutesa.
Muongozo wa kipengele cha upendo ni kwamba lazima wewe mwenyewe uanze kuwekeza kisha naye akupende.
Ni maisha ya ubinafsi kutaraji kupendwa wakati wewe huoneshi kwa mwenzako.
Zingatia hili kila siku na wakati wote ili uweze kufaidi matunda mema kwenye uhusiano wako.
Kuna tabaka la watu ambao huishi kwa kusikilizia zaidi. Haitakiwi kutegea, upendo unamaanisha pande mbili zinazovutana.
Huyu
anatekeleza hili kwa ajili ya mwenzake, hali kadhalika na
mwingine anasimama imara kuhakikisha mpenzi wake anafaidi malisho mema
ya huba.
Hakikisha mpenzi wako hakushindi upendo, onesha unampenda zaidi.
Upendo huyeyusha mengi. Ukiwekeza upendo kwa mwenzi wako, utamfanya nafsi yake iwe na woga.
Ni rahisi kushinda vishawishi, kama atakuwa akikaa peke yake atakuwa akijiridhisha kuwa unampenda kwa moyo wako wote.
Vinginevyo, anaweza kushawishika na kukusaliti kama tu akili yake itamtuma kuamini humpendi.
Hivyo basi, ...hakikisha upendo wako si wa wasiwasi. Mfanye awe na imani, ikibidi iwe ya kupitiliza.
Utafiti
unaonesha kuwa mtu aliyeonesha upendo mkubwa kisha akasaliti kwa tamaa
zake, anapobainika na kuachwa hujuta zaidi kuliko yule aliyeona hakukuwa
na upendo kwa sababu haoni cha kupoteza.
1.HOFU
Wengi hawajui hili. Unaweza kuwa na upendo mkubwa kwa mwenzi wako lakini kama huna hofu juu yake ni sawa na bure.
Katika kipengele hiki, nashauri watu kujitenga na maneno yasiyo na faida.
Mapenzi siyo tamko la kinywa peke yake, moyoni ndimo mahali pake.
Hii inamaanisha kuwa mapenzi hayatamkwi midomoni na yakaisha. Ni lazima mwili mzima uhusike kivitendo.
Mantiki
hapo ni kuwa unaweza kusema unapenda lakini kama huna hofu yoyote kwa
huyo umpendaye ni sawa na kupiga gitaa kumtumbuiza mbuzi, kwani
hakutakuwa na matokeo mazuri.
Faida
ya hofu kwenye uhusiano ni kuwa kila nukta, dakika, saa na siku,
utaishi kwa tahadhari. Lile ambalo unajua haliwezi kumpendeza mwenzi
wako, hutalitenda, hivyo kufanya maelewano kuwa makubwa
zaidi.
Husaidia kuepusha migogoro na kuumizana bila sababu za msingi.
Kiburi kimejikita kwenye vichwa vya watu wengi, hivyo kufanya hata yale ambayo wapenzi wao hawataki.
Mathalan,
mtu anaweza kutambua kuwa akivaa nguo za aina fulani, mpenzi wake
hawezi kufurahi lakini kwa sababu ya kutokuwa na hofu, anavaa na kuibua
ugomvi usio wa lazima.
Mtu
anajua kwamba mwenzi wake hapendelei tabia ya kutembea usiku lakini kwa
sababu ya kiburi, anasaga rumba mpaka usiku wa manane ndiyo anarudi
nyumbani. Ni kutafuta shari, hiyo ni tabia ya
kutopenda amani na mwenzi wako.
Sisemi uogope ila unatakiwa uwe na hofu kutoka moyoni.
Kila jambo linalotokea, hebu jiulize mara mbili mpaka tatu. Ukiona ni zito, jipe muda zaidi wa kutafakari kabla hujaamua.
Inawezekana ukalichukulia ni dogo, kumbe mwenzako akalitafsiri kwa
undani
zaidi, mwisho akaona muachane kwa sababu amehisi unamdharau. Zingatia
kwamba kufanya jambo la kumkera mpenzi wako kwa makusudi ni dharau.
Mimi
kama mchambuzi wa masuala ya mapenzi, nimegundua baada ya utafiti wangu
kuwa asilimia kubwa ya migogoro kwenye mapenzi hutokea kwa sababu ya
wawili wanaoamua kupendana kukosa hofu.
Hoja hapa ni kwamba ukiishi kwa kujiamini kupita kiasi mbele ya mwenzi wako ni janga. Ni sawa na kuuweka uhusiano wenu hewani.
Sina maana kuwa watu wasijiamini, mantiki ni kwamba kila mmoja ajipe hofu kwenye matendo yake ili asimkere mwenzake.
Ajue
kuwa dogo linaweza kuhatarisha mapenzi, kwa hiyo hatakiwi
kuthubutu kutenda. Uhusiano wa kimapenzi huunganisha pande mbili zenye
matarajio ya furaha, kwa hiyo ni vizuri kuishi kwa kuheshimu matarajio
hayo.
Lile ambalo unajua haliwezi kumpendeza mwenzi wako, hutalifanya, hivyo kufanya maelewano kuwa makubwa zaidi.
Husaidia kuepusha migogoro na kuumizana bila sababu za msingi.
Kiburi kimejikita kwenye vichwa vya watu wengi, hivyo kufanya hata yale ambayo wapenzi wao hawataki.
Mathalan,
mtu anaweza kutambua kuwa nikivaa nguo za aina fulani, mpenzi wake
hawezi kufurahi lakini kwa sababu ya kutokuwa na hofu, anavaa na kuibua
ugomvi usio wa lazima.
Mtu
anajua fika kwamba mwenzi wake hapendelei tabia ya kutembea usiku
lakini kwa sababu ya kiburi, unasaga rumba mpaka usiku wa manane ndiyo
unarudi nyumbani.
Ni kutafuta shari, hiyo ni tabia ya kutopenda amani na mwenzi wako.
Sisemi uogope, ila unatakiwa uwe na hofu kutoka moyoni.
Kila
jambo linalotokea, hebu jiulize mara mbili mpaka tatu. Ukiona ni zito,
jipe muda zaidi wa kutafakari kabla hujapata uamuzi sahihi.
Inawezekana
ukalichulia ni dogo, kumbe mwenzako akalitafsiri kwa undani zaidi,
mwisho akaona muachane kwa sababu amehisi unamdharau.
Zingatia kwamba kufanya jambo la kumkera mpenzi wako kwa makusudi ni dharau.
Kama
mchambuzi wa masuala ya mapenzi, nimegundua baada ya utafiti wake kuwa
asilimia kubwa ya migogoro kwenye mapenzi hutokea kwa sababu ya wawili
wanaoamua kupendana kukosa hofu.
Hoja hapa ni kwamba ukiishi kwa kujiamini kupita kiasi mbele ya mwenzi wako ni janga. Ni sawa na kuuweka uhusiano wenu hewani.
Sina maana kuwa watu wasijiamini, mantiki ni kwamba kila mmoja ajipe hofu kwenye matendo yake ili asimkere mwenzake.
Ajue
kuwa dogo linaweza kuhatarisha mapenzi, kwa hiyo hatakiwi kuthubutu
kutenda. Uhusiano wa kimapenzi, huunganisha pande mbili zenye matarajio
ya furaha, kwa hiyo ni vizuri kuishi kwa kuheshimu matarajio hayo.
UAMINIFU
Kifungu hiki kina vifungu vidogo viwili.
Mosi: Uaminifu binafsi. Yaani mhusika anakuwa anasukumwa kutorahisi mwili wake kutumika kiholela kutokana na kulinda heshima yake.
Hii
ina maana ya nidhamu binafsi. Nitoe msisitizo kwamba mwenzi bora wa
maisha ni yule anayejitunza kwa nidhamu binafsi. Nidhamu ya woga
inasaidia lakini si nzuri sana.
Pili: Ni uaminifu unaotokana na hofu.
Mtu
anakutana na vishawishi vya hapa na pale lakini anaogopa kuingia kwenye
uhusiano wa pili kwa sababu ya hofu aliyonayo kutokana na macho ya
jamii inayomzunguka.
Anajua watu wakijua watamuona mhuni (malaya), anataka aheshimike, kwa hiyo anabaki na uaminifu wake wa woga.
Katika
kipengele hicho cha woga, anaweza pia kuogopa kusaliti kwa sababu
anajua za mwizi ni arobaini. Anatambua kwamba ipo siku mwenzi wake
atajua na kuanzia hapo penzi ..litakufa.
Naye
hataki uhusiano wake ufe, kwa hiyo anajilinda, ingawa ndani yake
kunakuwa na msukumo wa kuanzisha figa la pili na tatu. Hata huu nao ni
uaminifu.
Ogopa mno mwenzi ambaye haoni cha kupoteza.
Huyo anaweza kukufanyia jambo baya wakati wowote.
Anaweza kuanzisha uhusiano mwingine katika kipindi ambacho bado unamhitaji.
Anaweza kukuacha na asijali maumivu yako. Hivyo basi, tazama uendako, mtathmini mwenzio kama ana sifa zinazofaa kisha
amua kwa faida yako mwenyewe.
HESHIMA Unahitaji
mpenzi ambaye anajiheshimu. Weka akilini hilo halafu lifanye kuwa
muongozo wa maisha yako ya kimapenzi. Heshima ina matawi mengi lakini
muhimu kwako ni kuwa lazima awe anakidhi vipengele vyote.
Wengi
wanateswa na mapenzi leo hii kwa sababu hawakuzingatia kipengele cha
heshima wakati wanaamua kuhusu hatma ya uhusiano wao.
Lazima awe anajiheshimu.
Nalilisisitiza hilo kwa mara ya pili kwa sababu kama hana heshima binafsi,maana yake hatakuwa nayo ya kumpa mwingine.
Watu wanaojiheshimu ndiyo haohao huwaheshimu wengine.
Nakuomba ulizingatie hilo kwa umakini mkubwa kwa sababu huamua furaha ya wapenzi, wachumba na hata wanandoa.
Mtu asiyejiheshimu anaweza kufanya jambo lolote na wakati wowote.
Anaweza pia kutoheshimu umuhimu wa mwenzi wake.
Tia
akilini kuwa mtu asiyejiheshimu huwa hana soni mbele ya macho ya jamii.
Anaweza kugombana na watu sehemu yoyote hata ukweni kwake.
Anaweza
kuvaa nguo za ‘kishenzi’ ambazo zitamuacha kwenye aibu mwenzi wake.
Yeye hawezi kuona aibu, kwani hajiheshimu. Binadamu wengi hujipa mizigo
mibaya kwa kuzoa watu ambao hawajui kujistahi, mwisho wanapata tabu
kuwarekebisha.
Wanasema, samaki mkunje angali mbichi, sasa wazazi na familia yake, walishindwa kumuweka sawa, wewe utawezaje wakati
ameshakubuhu? Tia akilini.
Post a Comment