Jaji mmoja wa
Marekani amesema kuwa mgombea wa urais wa chama cha Democratic, Hillary
Clinton lazima ajibu mashtaka yanayomkabili kuhusiana na matumizi mabaya
ya barua pepe kwa maandishi kuelezea hali ilivyokuwa alipokuwa waziri
wa maswala ya kigeni.
Kundi moja la wakereketwa wasiopendelea
mabadiliko, Judicial Watch, limeishtaki wizara ya mashauri ya kigeni juu
ya swala hilo likimtaka bi Clinton kutoa ushahidi binafsi chini ya
kiapo.
Shirika la upelelezi la FBI lilikamilisha uchunguzi wake
katika barua pepe hizo mwezi uliopita, bila kupendekeza mashtaka yo yote
dhidi ya bi Clinton.
Post a Comment