0


Apple wameamua kuja na matoleo matatu ya simu za toleo lake jipya linalotarajiwa kutoka hivi punde la iPhone 7 baada ya lile la iPhone 6 na 6 Plus kuzidiwa nguvu sokoni na Galaxy S7 Egde.

Katika tweet ya bwana Steve Hemmerstoffer ambaye mwandishi wamtandao wa NowhereElseFr, ambao ni maarufu kwa kuvujisha habari za mkampuni makubwa ametuma pich tatu za matoleo hayo.

Inasemekana iPhone 7 itakuja katika matoleo matatu ya iPhone 7, iPhone 7 Plus na iPhone 7 Pro. Picha kama hizi pia zimeonekana katika mtandao wa kijamii wa China, Weibo. Katika picha hizo, iPhone 7 Pro na iPhone 7 Plus zinaonekana kufanana kimaumbo japo inasemekana iPhone 7 Pro itakuwa na nguvu na vitu vingi zaidi.
iphone 7 
Apple inatarajiwa kuachia simu hizo katika mkutano wao wa Septemba maalumu kwa ajili ya kuachia matoleo mbalimbali ya vifaa vyao. Tetesi zinasema iPhone 7 itakuja na RAM ya 3GB na kioo cha QHD au 4K na processor ya hexa-core.

Post a Comment

 
Top