0




 Mbunge wa jimbo la Liwale,Mh.Zuberi Kuchauka akiongea na wananchi wake katika mkutano wa hadhala uliofanyika jana katika uwanja wa Nanjinji uliopo kijiji cha Likongowele kata ya Likongowele Liwale mjini


wananchi wa jimbo la Liwale wakiwa wakiwa kw enye mkutano wa mbunge wao uliofanyika jana katika uwanja wa Nanjinji
 Mbunge akinukuu maswali mbalimabili ya wananchi waliouliza ili kupatiwa majibu
 Mwenyekiti wa chama cha walemavu wilayani Liwale,Bwana Mshamu Mulue akiuliza swali
 Bwana Hasani Makuche mmoja ya wananchi waliopata nafasi ya uliza swali hapo jana
 Imani Mtesa aliyekuwa mgombea wa ubunge jimbo la Liwale kupitia ACT nae alipata nafasi ya kuuliza swali kwa mbunge wake
 Bi. Somoe Kujakila aliweza kupata nafasi ya kuuliza swali lilohusu mambo ya huduma ya afya katika hospitali ya wilaya wa Liwale
 Mohamedi Ngotwike nae aliweza kupata nafasi ya kuuliza swali juu ya majibu ya serikali aliyopewa mbunge wake baada ya mbunge Kuchauka kuuliza maswali mbalimbali akiwa bungeni
 Othumani Mkomba aliweza kupata nafasi ya kuuliza swali kwenye mkutano huo wa hadhala
  Mshamu Tewele aliweza kupata nafasi ya kuuliza swali kwenye mkutano huo wa hadhala 


Mbunge wa Jimbo la Liwale,mh Zuberi Kuchauka (Cuf) amewata vijana kuchangamkieni fursa zilizopo wilayani hapa ili kuweza kujikwamu na umasikini.

Hayo aliyasema Jana kwenye mkutano wa adhara uliofanyika katika uwanja wa mkutano wa Nanjinji katika kijiji cha Likongowele kata ya Likongowele wilayani Liwale mkoani Lindi.

 Kuchauka alisema wilaya ya Liwale kuna fursa nyingi sana lakini utambuzi wa fursa zilizopo ni mdogo hivyo kinachotakiwa vijana kuwa tayari kuunda vikundi mbalimbali vya ujasiliamali ili kuweza kuchangamkia fursa zilizopo alizitaja baadhi ya fursa zinazopatikana wilayani hapa kama vile ufugaji wa kisasa wa nyuki,ufugaji na kilimo na aliongeza kusema serikali ya awamu ya tano alihadi kutoa fedha kila kijiji shilingi milioni 50 hivyo pesa hizo zitagawiwa kwenye vikundi za ujasiliamali.

 Pia Kuchauka aliwata wananchi kuwatumia vema maafisa ugani waliopo katika shughuli zao mbalimbali za kimaendeleo kama kilimo,ufugaji wa kuku na wanyama na ufugaji wa nyuki ili kuweza kuongeza kipata.

 "Ni ajabu sana kuona maafisa ugani na mifugo wapo hapa wilayani lakini hatuwatumii alafu wanachukua mishahara na ajabu kuona afisa ugani hana shamba la mfano na hawawatembelei wakulima kwenye mambasha yenu"alisema Kuchauka.

Kuchauka aliweza kubainisha suala la fidia kwa wananchi ambao mazao yao yakishambuliwa na  wanyapori alisema tatizo kubwa la wananchi hawafahamu sheria ya jinsi ya kudai na kupata fidia zao lakini serikali inafahamu na kuna kiwango maalumu kwa kila hekta na umbali wa kutoka shamba mpaka hifadhi sasa kinachotakiwa mkulima anatakiwa atoe taarifa kwa mtendaji wa kijiji ndipo hizo taarifa kufikishwa sehemu husika.

Bi Somoe Kujakila aliweza kuuliza swali kwa mbunge kuna kero sana kwa akinamama wajawazito wakati wa kujifunguo katika hospitali ya wilaya na dawa hakuna ,Kuchauka alijibu kwa kusema kuwa  kero hiyo naifahamu sana na moja ya hotuba yake ya kwanza bungeni aliongelea kero hiyo ana alisema wilaya ya Liwale haina hospitali ya wilaya bali kuna kituo tu cha Afya na ameomba akinamama waendelee kuvumilia na kusema wahudumu wa afya waliopo ni wachache sana na kusema bajeti hii ikisaidia inaweza kupunguza kero hiyo.

Mohamedi Ngotwike nae alipata nafasi ya kuuliza swali kwanza nakupongeza kwa harakati zako ulipokuwa unachangia sana na unauliza maswali bungeni lakini hatujapata majibu ya maswali uliokuwa unayauliza Kuchauka alisema majibu ya mawaziri yapo kwenye vitabu ambazo waligawiwa hivyo anaandaa utaratibu wa kuweka kituo binafsi ili kuwapa wananchi vitabu ili waweze kusoma na kufahamu mambo mbalimbali pia aliongeza kusema wanaliwale waanzishe utaratibu wa kuanzisha kituo cha sheria ili kuweza kuwapa msaada wa kisheria wananchi.

Post a Comment

 
Top