0
Ni moja ya barabara ya kuelekea katika ofisi ya chama cha bodaboda

Baadhi ya viongozi wa chama cha bodaboda kama m/kiti Bw.Rafii Likochelo na wajumbe wakisimamia ujenzi wa ofisi ya chama cha bodaboda iliyopo katika kijiji cha Mungurumo karibu na ofisi za Idara Maji wilaya
 Hii ndio ofisi cha chama cha bodaboda ujenzi wake ukiendelea kukamilika



Katika harakati za kujikwamua na umasikini kwa vijana chama cha waendesha tax,bajaji na pikipiki (bodaboda) cha wilayani Liwale mkoani Lindi kilianza rasmi mwaka 2014 kikiwa na wanachama 65 hadi sasa mwaka 2016 kina jumla ya wanachama 300.

Chama cha hiki kwa kushiriana viongozi wa chama na wanachama kimeweza kukopesha pikipiki  65 na vifaa mbalimbali vya ujenzi kwa wanachama wake toka mwaka 2014 hadi februaru 2016.

Kila kazi mara nyingi au hulenga na fanyikio,katika chama hiki cha bodaboda kimeweza kufanyikiwa kwa kuweza kupata mambo mbalimbali kwa ushirikiano na viongozi mbalimbali wa kisherikali na viongozi wa vyama vya ushirika na wafanyabiashara walioko ndani ya wilya ya Liwale.

Baadhi ya mafanyiko ya chama cha bodaboda ni
Kimeweza kuongeza matawi ya wanachama wa bodaboda kutoka matawi 4 mpaka sasa kuwa na matawi 7 baadhi ya matawi hayo yapo vijijini kama vile Likombola na Mpengele.

Kumiliki uwanja  na kujenga ofisi ya chama kwa ushirikiano na viongozi mbalimbali wa serikalini na wadau wengine waliowezesha chama kupata uwanja na kujenga ofisi.

Kupata mikopo kutoka serikalini ya asilimia 5 (5%) ya vijana.

Richa ya kuwa na ma kufanyikiwa  zipo changamoto wanazokumbana nazo kama vile
Uwezeshaji mdogo wa kifedha katika chama cha bodaboda hivyo hushindwa kuendesha shughuli mbalimbali za kichama kwa wakati hivyo hutegemea michango yao lakini haimalizi mahitaji
Usumbufu wa askari barabarani baada ya viongozi walibainisha kuwepo kwa usumbufu kwa baadhi ya askari polisi kuwasumbua waendesha bodaboda.

Kunyang`anywa kwa pikipiki,viongozi walibainisha toka chama kianzishwe rasmi mwaka 2014 mpaka mwaka 2016 kumetokea na kuuawa kwa mwanachama wao mmoja  na kung`ang`anywa pikipiki 6.

Chama cha bodaboda kina ushirikiano mzuri kati ya chama na viongozi mbalimbali wa serikalini ikiwemo na Mkuu wa wilaya ya Liwale mh. Ephraim Mmbaga aliweza kuwaunganisha wanachama wa bodaboda baada ya chama hiko kuingia kwenye mpasuko.

Mbali ya kuwaunganisha wanachama mkuu wa wilaya mh. Mmbaga alikisaidia chama cha bodaboda mawazo chanya na kusaidia chama kupata  mkopo wa pikipiki na uwanja wa ofisi na ujenzi wa ofisi ya chama cha bodaboda.

Nae mbunge wa jimbo la Liwale, mh. Zuberi Kuchauka ameonesha ushiriano wake kwa kuwaweza vijana hao kuwapatia fedha za mfukom wa jimbo kiasi cha shilingi milioni 2.5 kwa ajiri ya kuendeleza ujenzi wa ofisi ya chama cha bodaboda.

Wapo wafanyabiashara walionesha kushirikiano mkubwa na msaada kwa vijana wa chama cha bodaboda  kama Amidu Wamo ambaye amewakopesha chama cha bodaboda pikipiki 42 na chama hurejesha malipo kidogo kodogo na kwa awamu.

Baadhi ya wadau wengine wameweza kukisaidia chama cha bodaboda kama chama cha ushirika umoja pamoja na mwenyekiti wa chama hiko Bw. Hasani Mpako kwa kuweza kuchangia bati 20 pamoja na chama cha ushirika Umoja kiliweza kuchangia pia bati 20 za ujenzi wa ofisi ya bodaboda na baadhi ya viongozi wengine waliosaidia chama kwa namna moja pamoja na  ofisi ya Maendeleo ya jamii Wilaya na seluu.

Post a Comment

 
Top