0


            Kaimu Ligoma wa pili kutoka kushoto na Jonson Mpilimba wa pili kutoka kulia





                    kusho ni Yahaya Husseni na Mukisini Kinderu wa pili kutoka kulia
Mgeni rasmi Bw.Hassani Mpako akiongea na wadau wa masumbi mara baada ya kumalizika kwa pambano.
Jana wakazi wa wilayani Liwale mkoani Lindi walishudia mipambano miwili mkali sana ya ngumi (Boxing) iliyowakonga yoyo za washabiki  wa mchezo wa masumbi kwani kulikuwa na ugeni kutoka jijini Dar es salaam kuja kupambana na mabondia wa Liwale.

Katika mchezo wa kwanza wa masumbi uliofanyika jana usiku katika ukumbi wa LENAR CLUB uliwakutanisha bondia kutoka Liwale Kaimu Ligoma Vs Jonson Mpilimba kutoka jijini dare s salaam ambao uzito wao ulitofautiana Ligoma alimzidi Mpilimba uzito wa kila 6.

Mpambano huo ulikuwa na Round 6 mwazo wa mchezo katika roundi ya kwanza kila mchezaji aliweza kumsoma mwezake jinsi mbinu anayotumia na kusoma makosa ya mwezeke,roundi ya 3 na ya 5 mpambano ulikuwa mkali sana kwani kila mtu alikuwa yupo makini sana huku mashabiki wakiwa na kiu ya kumfahamu nani atashinda juu ya pambano hilo.

Roundi ya 5 Kaimu Ligoma aliitumia vizuri baada ya kumpunguza nguvu Jonson Mpilimba kwa mtwanga makonde maziko na Mpilimba kupelekea kushindwa kuimili hayo makonde lakini alijikakamua mpaka kumaliza roundi hiyo ya 5.

Katika roundi ya 6 hapa mpambano ndio ulikuwa mkali zaidi huku bondia Kaimu Ligoma alishangiliwa na mashabiki wengi  ambao kelele zile zilimfanya aongeze juhudi zaidi ya kushinda kwani ikizingatia wakazi wengi walienda kuona ndugu zao watawashinda watu wa jijini Dar es salaam kitendawili hiko kiliweza kuteguliwa namo roundi ya 6 baada ya Ligoma kumtandika Jonson Mpilimba na majaji wa mchezo huo waliweza kutoa pointi 

Jaji wa kwanza aliweza kutoa pointi kama ifuatayo-;
1.       Kaimu ligoma alipewa pointi 51-29 Jonson Mpilimba
2.       Kaimu ligoma alipewa pointi 51-29 Jonson Mpilimba
3.       Kaimu ligoma alipewa pointi 51-29 Jonson Mpilimba
Kwa matokeo haya Kaimu Ligoma kutoka wilayani Liwale alitangazwa mshindi wa pambano hili.

Pambano la pili likafuata nalo nilikuwa linasubiliwa kwa hamu sana baada ya kuwakutanisha mkongwe wa masumbwi kutoka hapa wilayani Mukisini Kinderu Vs Yahaya Husseni kutoka jijini Dar es salaam huu mchezo ulikuwa na jumla ya  round 8.

Mchezo huu ulichezwa katika round 3 tu na mshindi akatangazwa katika roundi ya kwanza na ya pili mchezo ulikuwa mzuri sana kwani kila mmoja alionesha uwezo wake mbele ya mashabiki waliojaa ndani ya ukumbi wa LENAR CLUB na kuweza kukonga nyoyo za mashabiki wa ngumi.

Katika roundi ya 3 bondia Mukisini Kinderu aliweza kuonesha uwezo wake mbele ya mashabiki waliofika uwanja hapa baada ya kupiga mpizani wake Yahaya Husseni na kupelekea  bondia Yahaya kugeguta mkono na kushindwa kuendelea na mpambano huo ndio majaji waliweza kumtangaza mshindi bondia Mukisini  Kinderu na kuwafanya wapenzi wa masumbi hususani wakazi wa Wilayani Liwale kujawa na furaha zaidi baada ya wachezaji wao kuweza kushinda mapambano yao yote.

Mara baada ya kumalizika kwa mpambano washiriki wote waliongea na Mwandishi wa habari wetu kuzungumzia juu ya mchezo huo kwa pande zote zili pamoja na waliwalimu wao nao walihojiwa.

Bondia Jonson Mpilimba alisema amekili kushindwa kwenye mpambano wake dhidi ya mpinzani wake Kaimu Ligoma japo alizidiwa uzito wa kila 6 lakini aliongeza kusema anajipamba upya na kama kutakuwa na pambano lijalo ataweza kushinda nae Kaimu Ligoma alisema amesikia furaha zaidi kuitanza Liwale kwa ushindi alioupata pia alibainisha siri ya ushindi wake ni kushiriki mazoezi na kuzingatia maelekezo ya mwalimu na kusema mchezo wa bondia si mchezo wa kubezwa kwania ni moja ya mchezo wa kujenga afya ya mwili na amewaomba wadau mabalimbali kujitokeza kuweza kusaidia mchezo huo.

Mukisini Kinderu alisema huu ushindi ni zawadi tosha kwa wakazi wa Liwale hii kwani vijapaji zipo na watu wa wialayani wanavipaji  amewaomba viongozi na wadau kuweza kuzamini mashindano mabalimbali ili kuweza kutoa fursa na kujenga ushirikiano nae bondia Yahaya Husseni alisema pambano hili ameshindwa na kilichotoa ndio matokeo ya mchezo lakini hakati tamaa ataendelea kujipanga na anatamani kukutana nae Kinderu kwa pambano jingine.

Mbwana Amdani ni kocha  wa mabondi  Jonson Mpilimba na Yahaya Husseni wa kutoka jijini Dar es salaam alisema mchezo wa jana ulikuwa mzuri japo wanafunzi wake wameshindwa mapambano yote lakini ataweza kuboresha makosa yaliotokea kwa mwanafunzi  pia aliongeza kusema kila siku akiomba pambano na Mukisini Kinderu siku zote kideru huwa anamkimbia aliopoulizwa na mwandishi wetu bondia Kinderu alikataa madai hayo na kusema yeye amuogopi na yupo tayari kupambana nae.

Nae kocha wa mabondia kutoka wilayani Liwale Amiri Kolela na mzamini wa pambano hilo alisema mchezo ulikuwa mzuri na siri ya kushindi walisema walijiandaa kwa ndani ya miezi 3 kwani hakutaka kufanya vibaya kwakuwa mpambano huo unafanyika nyumbani,ushindi waliopata ni zawadi tosha kama vijana wa Liwale wanauwezo mkubwa.

Kolela alitoa wito kwa vijana wajitokeze kushiriki katika michezo yote ili kujenga afya pia alibainisha kama vijana watashiriki katika mchezo matumizi ya madawa ya kulevya yataisha na vijana watakuwa na mawazo chanya ya kimaendeleo pia michezo ni kitu muhimu sana kwani mchezo hujenga urafika katika maeneo mbalimbali ya nchini.

Kolela aliweza kubainisha changamoto mbalimbali za mchezo huo alizitaja baadhi ya changamoto kama vile kukosa sapoti kwani wanatamani kufanya mapambano mengi sehemu mbalimbali lakini inashindikana baada ya kukosa sapoti hivyo amewaomba wadau wa michezo kujitokeza kuweza kusapoti mchezo huo kwa kila mchezo unafaida na ni ajira.

Changamoto ingine ni uhaba wa vifaa vya michezo amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kuweza kuwasaidi ili waweze kufanya mazoezi zaidi lakini japo kuwa kuna uhaba wa vifaa na changamoto hawakati tamaa wanaendelea na mazoezi.

Mgeni rasmi wa pambano hilo ni mwenyekiti wa chama cha ushirika Umoja Mh.Hasani Mpaka alisema yupo tayari kutatua changamoto zinazowakabili wanabondio hao hivya amewaahadi kuwapatia baadhi ya vifaa muhimu vinavyohitajika  muda huu alionfgeza kutoa ahadi atazami pambano moja kubwa ili vijana kuweza kuonesha vipaji vyao na kuweza kuwashawishi vijana mbalimbali kupenda michezo na kuona faida ya watu kushiriki katika michezo.

Pia amewatoa wasiwasi wanabondia na mashabiki wote walioudhulia mchezo huo juu ya bondia Yahaya Huseni aliyeteguka mkono atamlipia huduma zote za matibabu.




Post a Comment

 
Top