Rais Zuma anasema nia yake kuu ya kuitisha uchaguzi huo wa mashinani mapema ,ni kutathmini umaarufu wa chama chake cha ANC kufuatia tuhuma kuwa amepoteza uhalali wa kuiongoza taifa hususan baada ya kupatikana na hatia ya kupuuza maamuzi ya mahakama ya taifa hilo.
Zuma aliwataka wenyeji wajiandikishe kuwa wapiga kura kwa wingi iliwathibitishie upinzani kuwa kweli Afrika kusini imekomaa kidemokrasia.
Hii leo vyama vya kupigania haki za kibinadamu visivyo vya kiserikali vimejiunga na wale wanaomtaka ajiuzulu wadhfa wake vikisema amepoteza uhalali baada ya uamuzi huo wa mahakama ya juu.
Wengine waliomkaripia rais Zuma na kumtaka ajiuzulu ni aliyekuwa jaji wa mahakama ya juu Zac Yacoob, balozi mstaafu wa Afrika kusini nchini Uingereza Cheryl Carolus, kiongozi wa vyama vya wafanyikazi Zwelinzima Vavi kwa mujibu wa jarida la News24.
Tawi hilo ndilo linalokabiliwa na ushindani mkubwa zaidi kutoka upinzani kwani wenyeji wake wamekuwa wakiwasikiza sana viongozi wa upinzani wakiongozwa na Julius Malema wa chama cha EFF.
Hata hivyo matawi mengine ya chama tawala ANC, ikiwemo lile la wanawake na pia la vijana yangali yanamuunga mkono rais Zuma.
Zuma amekiri makosa yake na amekubali kulipa fedha zote zilizotumika kufanyia ukarabati makaazi yake ya Nkandla.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.