Na Mwandae Mchungulike
LIWALE-LINDI
Gari ya jeshi la Polisi lenye namba PT 3704 Land cruiser (mpya) la kituo cha polisi wilayani Liwale
mkoani Lindi limeacha njia na kupinduka na
kujeruhi watu 6 maeneo ya kata ya Mungurumo tarafa ya Liwale mjini katika barabara
ya Kichonda majira ya saa 8 mchana february 2 leo .
Gari hiyo ikiwa inatoka katika kijiji cha Kimambi kumchukua
mke wa askali Muddy ambaye alilala njiani tangu jana akiwa kwenye basi akitokea
jijini Dar es salaam baada ya basi hilo kukwama umbali wa kilometa 40 kufika
Liwale mjini,ilipokaribia kuingia mjini gari iliteleza na kuacha njia kisha kupinduka
na kusababisha majeruhi ya watu 6 waliokuwa wameomba msaada kwenye gari ambao
wamepata majeraha na michubuko sehemu mbalimbali ya miili yao.
Kamanda wa polisi wilaya ya Liwale Raphael Mwandu amesibitisha
kutokea kwa ajali hiyo na alisema majeruhi
wamepatiwa matibabu na hali zao wanaendelea vizuri.
Kamanda Mwandu amewataja waliojeruhiwa katika ajali hiyo ni
askali na dereva wa gari hiyo Desdery (45),Ubaya Kandros Mwingira (32) dereva
na mkazi wa Kata ya Nangando liwale mjini,Ramadhani Saidi Kaselewenje (23)
mkulima na mkazi wa Keko-Dar es salaam,Hassani ALLY Ponela( 26) mfanyabiashara
na mkazi wa Dar es salaam,Ally Mussa Ahmad mfanyabiashara na mkazi wa uwanja wa
ndege Dar es salaam na Shabani Othmani Lugume (40) mfanyabiashara na mkazi wa
Kongowe Dar es salaam.
Pia kamanda huyo alisema gari hilo baada ya kupata ajali bado
zima ila kioo cha mbele kimepata nyufa.
KUANGALIA TASWIRA YA BARABARA YA LIWALE TO NANGURUKURU>>> BOFYA HAPA
KUANGALIA TASWIRA YA BARABARA YA LIWALE TO NANGURUKURU>>> BOFYA HAPA

Post a Comment