Rais wa Burkina
Faso amesema takriban watu 21 wameuwawa katika shambulio kwenye hoteli
moja mjini Ogadugu na wanamgambo waliovamia hotel hiyo.
Roch Mark
Christian Kabore amesema washambuliaji wanne waliovamia hotel hiyo
waliuliwa ambapo wawili kati yao ni wanawake. Shambulio hilo lililotokea
kwenye hotel ya Splendide kwenye mji mkuu wa Ouagadougou sasa
limemalizwa.walionusurika wanasema wanamgambo hao walianza kupiga risasi kwenye jengo hilo na kisha kuliwasha moto.
Watu 126 waliokuwa mateka waliachiliwa huru katika hoteli ya Splendid iliopo katika mji mkuu wa taifa hilo la Magharibi mwa Afrika Ouagadougou, kwa mujibu wa waziri wa maswala ya ndani.
Vikosi maalum vya Ufaransa vinasaidia wanajeshi wa taifa hilo katika oparesheni hiyo.
Kundi la Al-Qaeda la islamic Maghreb{AQIM} limesema kuwa lilitekeleza shambulio hilo katika taifa hilo la Magharibi mwa Afrika.
Post a Comment