ITV imeshughudia jeshi la polisi likimtoa kwanguvu mbunge wa jimbo
la Kilombero baada ya kuamuriwa na mwenyekiti wa kikao Bw. Yahya Nania
kwa madai ya kwamba Simjumbe halali wa kikao hicho ambapo mvutano mkubwa
ulitokea na mambo yalikua hivi.
Akizungumza baada ya mwenyekiti kutoa agizo la kutolewa mbunge huyo
mbunge wa jimbo la Mlimba Suzan kiwanga amesema hakuna sheria
inayoruhusu kumzalilisha kiongozi huyo kwa kumtoa kwa nguvu kwakuwa ni
mjumbe halali wa kikao hicho na alichaguliwa na wananchi wa Kilombero
kuwa mbunge wao.
Naye mbunge wa jimbo la Kilombero Peter Lijualikali akizungumza
mara baada ya kutolewa nje amelaani kitende hicho alichofanyiwa ambapo
ameitaka serikali kuingilia kati swala hilo na kwamba swala hilo
lisipofanyiwa ufumbuzi ataenda mahakamani ili haki itendeke huku mjumbe
wa kanda Chadema Methew Likwina akiomba serikali kuingilia kati swala
hilo vinginevyo kuwepo na uchaguzi mwingine wa mji mdogo wa Ifakara kuwa
jimbo.
Vurugu hizo zilisababisha mwenyekiti wa kikao kuahirisha kikao kwa
saa mbili na wajumbe walivyo rudi kwa mara ya pili hapakuwa na
chakuongea ambapo aliahirisha kikao hadi kitakapo tangazwa tena.
Post a Comment