0
 
Tangazo kuhusiana na jaribio hilo la bomu la Hydrogen la Korea Kaskazini
Siku moja baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la bomu la haidrojeni, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekubaliana kuanza mikakati ya kuiwekea vikwazo.
Hata hivyo baadhi ya Wataalamu wameonyesha kuwa na wasi wasi kuhusu jaribio la sasa la nyuklia la Korea Kaskazini ambalo ni la nne katika mwongo mmoja, wakisema huenda lisiwe la haidrojeni kutokana na mlipuko uliotokea.
Bomu la hydrojeni ni moja ya mabomu hatari ya jamii atomiki au nyuklia yenye nguvu zaidi. Wataalam wanasema bomu hili la hydrojeni lina uwezo mkubwa kiasi kwamba linaweza kulipua mji mmoja wote kwa mlipuko mmoja.
Kufuatia jaribio hilo jamii ya kimataifa imendelea kulaani tukio hilo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Waziri wa zamani wa Mambo ya nje ya Korea Kusini Ban Ki moon akisema jaribio hilo la bomu la nyuklia ni hatua ya kuogopesha.
"Hili jaribio kwa mara nyingine limekiuka maazimio kadhaa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pamoja na wito wa pamoja wa jamii ya kimataifa kukomesha vitendo hivyo. Pia linakwenda kinyume kabisa na utamaduni wa kimataifa wa majaribio ya mabomu ya nyuklia. Tendo hilo linaonekana ni la kuogopesha kwa usalama wa kanda na kupuuza juhudi za kimataifa za kuacha kutengeneza silaha za nyuklia. Ninalaani kwa nguvu jambo hilo." >>>>> KUENDELEA KUSOMA BOFYA HAPA

Post a Comment

 
Top