0


Serikali imesema haitauza nyumba yoyote ambazo zimepangishwa zamani kwa  wananchi kupitia shirika la nyumba la taifa ambazo azipo katika miradi ya maalumu wa ujenzi wa nyumba na kuuza ikiwa njia moja wapo ya kuhakikisha wananchi wa kipato cha chini waweze kuendelea kusaidiwa na serikali katika makazi.

Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi wiliam Lukuvi amesema hayo akiwa mkoni morogoro ambapo amesema sera ya uuzaji wa nyumba za serikali na za shirika la nyumba ambazo zinatumika kwaajiri ya upangishaji aitakuwepo kwa serikali ya awamu  ya tano inayoongozwa na rais john pombe magufuli.

Akiwa mkoni morogoro waziri huyo wa ardhi alifungua ofisi ya hati ya kanda ya mashariki ambayo itahudumia mikoa ya pwani na morogoro ili kuweza kuraisisha huduma ya utoaji wa hati huku akiaidi kuendela na mchakato wa kutoa huduma kwa njia ya electoniki kwa nia ya kupunguza migogoro ya ardhi.

Post a Comment

 
Top