Mwanajeshi akikabiliana na wavamizi wa hoteli ya Splendid nchini Burkina Faso
Oparesheni ya
kuizunguka hoteli moja iliovamiwa na wapiganaji imeisha ,serikali
imetangaza,lakini ripoti zinaarifu kwamba hoteli nyengine iliopo karibu
imeshambuliwa.
Watu 126 waliokuwa mateka waliachiliwa huru katika
hoteli ya Splendid iliopo katika mji mkuu wa taifa hilo la Magharibi mwa
Afrika Ouagadougou, kwa mujibu wa waziri wa maswala ya ndani.Vikosi maalum vya Ufaransa vinasaidia wanajeshi wa taifa hilo katika oparesheni hiyo.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande ameshtumu shambulio hilo la taifa hilo ambalo lilikuwa koloni yake hapo zamani.
Mnamo mwezi Novemba shambulio la AQIM katika hoteli moja ya Bamako nchini Mali liliwauwa watu 19.
Post a Comment