Mbunge wa Jimbo la Liwale,Zuberi Kuchauka akifuatilia kwa ukaribu matengenezo ya X-ray katika Hospitali ya Wilaya ya Liwale.
Halmashauri ya wilaya Liwale imeanza kufanyia matendengezo ya X-ray ambayo iliyosimama kwa muda wa zaidi miezi tisa na kupelekea wagongwa wanaohitaji vipimo vya x-ray kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hiyo.
Hayo yameelezwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Gaudence Nyamihula wakati alipokuwa anazungumza na timu ya waandishi wa habari waliotembelea wilayani humo.
"Uongozi wa wilaya
ulifanyamawasiliano na wizara ya
afya na kupatiwa fundi kutoka Kampuni ya Philips ambayo ndiyo yenye mkataba
wa kufanya matengenezo ya mashine hizo.
Nyamihila alisema mashine hiyo ilikuwa na tatizo la kufa
betri na itilafu zingine za
kiufundi lakini kipindi hiki mashine hiyo inatendenezwa ili wagonjwa wanaohitaji
vipimo hivyo waweze kwenda kupatiwa huduma katika hospitalini hapo.
Kwa upande wake
Mganga mkuu Dkt Maltin alisema
Hospitali ya wilaya inakabiliwa na changamoto
ikiwemo upungufu wa watumishi damu salama, dawa, vifaa tiba, uchakavu wa
majengo na eneo la kutenga watu wenye magonjwa ya kuambukiza ukiwemo
Kipindupindu.
Alisema mbali ya
upungufu huo, wapo baadhi ya watumishi hasa wauguzi ambao kuacha kazi muda
mfupi baada ya kuajiriwa kutokana
mazingira ya kijiografia ya wilaya
na kuongeza upungufu zaidi.
Nae Mbunge wa jimbo la Liwale, Zuberi kuchauka alisema
tatizo la X-ray limekuwa kero kwa wananchi na wagonjwa katika wilaya hiyo kutokana na kutumia fedha
na muda mwingi kuangaikia huduma hiyo nje ya wilaya.
Post a Comment