0


Picha imepigwa akiwemo kocha wa Arsenal, Nwankwo Kanu na wachezaji Nwakali na Samuel Chukwueze. Picha hiyo imepigwa kwenye ofisi za makao makuu ya club ya Arsenal ambapo wamekutanishwa na kocha huyo wakielekea ku-sign kwa ajili ya kucheza Arsenal.

Wote wawili wana umri wa miaka 17 na wamefuatiliwa na Arsenal wakati wa kombe la dunia la chini ya miaka 17 ilifanyika Chile. Wote wawili wanategemewa kuwekwa kwenye mpango wa vijana wa Arsenal ili kujiendeleza na kabla ya kujiunga na timu ya wakubwa.

Baadhi ya wachezaji waliopitia hatua kama hii ni Cesc Febregas ambae aliingia akiwa na miaka 15.

Post a Comment

 
Top