0



                        Philimon Kaspal Punda akiwa kwenye eneo la tukio shambani
                   korosho waliokuwa wameziokota kutoka shamba lao la mikorosho
Philimon Kaspal Punda aliyekaa katikati akipewa msaada wa usafiri

Kijana mmoja anayefamika Limu Philimon Punda mwenye umri wa miaka 18 amemua mama yake mzazi bi Christina Raymond Mposa mwenye umri wa miaka 41 kwa kumchoma kisu kwenye ziwa na kufaliki hapohapo na kumjeruhi baba yake mzazi Philimon Kaspal Punda shambani kwao majira ya saa 3 usiku jana katika kijiji cha Tepetepe kata ya Mungurumo wilayani Liwale mkoa wa Lindi.

Tukio hili la kikatili lilitokea katika  shamba la mikorosho kwa wazazi wa Limu punda ambaye aliyefanya ukatili huu wakiwa katika shughuli za kilimo za kuokota korosho ghafla alikuja mtoto wao Limu Punda na kuanza kumshambulia baba yake Philimon Punda na kumjeruhi usoni maeneo ya jicho la kushoto na mkononi karibu na begani na baada ya kufanya tukio kijana huyo kutokomea kusikojulikana .

Mashaka Punda ambaye mtoto wa Philimon ambaye shuhuda wa tukio alisema baada ya  kaka mtu anamsha baba yao ndipo mama yao kwa sasa marehemu alienda kuamua ugomvu ndipo alipochomwa kisu kwenye ziwa na kufaliki hapohapo ndipo baba na watoto wake wawili kuelekea kwa majirani kuomba msaada.

Philimon Punda yupo kwenye hospital ya wilaya ya Liwale akiwa anapata matibu baada ya kuvujwa damu nyingi.

Katika tukio lingine Limu Punda majira ya saa moja karo usiku alimjeruhi bi Hajra Ally Nyimage mkazi wa kijiji cha mungurumo kata ya Liwale mjini ambaye ni  mwanafunzi  wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Rashidi Mfaume Kawawa(R.M) 

Hajra nyimage akiongea na mwandishi wa habari kwenye hospital ya wilaya ya Liwale akiwa kwenye matibabu leo  alisema kijana huyo leo siku ya pili kuja  kujeruhi siku ya kwanza ilikuwa mwezi uliopita arimjeruhi na jana alimjeruhi mkono wa kushoto sehemu mbili na mkono wa kulia kwenye kidole na ameshonwa nyuzi sita.

Kamanda wa polisi wa wilaya ya Liwale Rapheal Mwandu amethibisha kutokea kwa matukio haya mawili na jeshi lake linasaka Limu Punda aliyefanya ukatili huo ili kumfikisha kwenye mkono wa sheria.

Post a Comment

 
Top