0



Ajali ya pikipiki imemgonga mpanda baiskeli Mshamu Salum Majura(80) na kusababisha kifo ajali hiyo imetokea leo decemba 29 majira ya saa 8 mchana  katika kijiji cha Mbaya kata ya Mbaya wilayani Liwale mkoani Lindi.

Mwendesha pikipiki na  mkazi wa kijiji cha Mbaya Miraji Rajabu Kauka (22) aliokuwa akiendesha pikipiki yenye namba T599DE aina ya SANLG alimgonga Majura maeneo ya kichwani na mkono wa kushotona kufariki dunia.

Kamanda wa polisi wilaya ya Liwale Raphael Mwandu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na alisema mtuhumiwa amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Liwale na hali yake ni mbaya.

Post a Comment

 
Top