0
Zaidi ya shilingi milioni 30 zimetumika kwa ajili ya kukarabati wordi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mtwara Ligula
Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika hospitali ya rufaa Ligula, Mkurugenzi mtendaji wa Ecobank Tanzania, Enoch Osei-Safo alisema benki yake imekuwa ikisherekea Siku y aecobank nchini Tanzania kwa kufanya matendo matukio ya  na mambo ya kuthamini jamii inayoizunguka.
Alisema taifa la kesho lipo mikononi mwa watoto  Kwa kulitambua hilo wameamua kutoa msaada wa kukarabari wodi ya  watoto hao ili waweze kukua vizuri  na kuwa na nguvu lazima  wapata aafya bora.
Tunatambu ataifa la kesho lipo mikononi mwa watoto wetu. Kwa kuhakikisha tuna wapatia afya bora, watoto watakua wenye nguvu na ushupavu tayari kwa kukabiliananaDunia”alisema Osei-Safo
 Kwa upande wake mgeni rasim Kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara ambaye pia mkuu wa wilaya ya Mtwara mjini, Fatma Ally aliyekuwa mgen irasmi washughuli hiyo aliwapongeza Ecobank Tanzania kwa moyo wao mkunjufu katika kukarabati wodi ya watoto na kujitolea muda wao kukaa na watoto hao waliokuwa wamelazwa wodini hapo.
Fatma aliihimiza benki hiyo kupanua wigo wa uhisani wao  katika sektayaElimu, Mazingira, Kilimona masuala mengine yanayo kabili jamii moja kwa moja na akawahakikishia kuwa serikali itaendelea kuboresha hudumaza afya katika hospitali mbalimbali, elimu na mazingira mkoa mzima.
NayeKaimu Mganga mkuu wa hospitali hiyo  Joseph Mweru aliipongeza benki hiyo kwa mchango wao na kusema ukarabati huo utasaidia kupunguza vifovya watotowa change ambao hupoteza maisha yao kwa kukosa mazingira safi, salama na hewasafi.
Takwimu zinaonyesha vifo vya watoto mkoani Mtwara mwaka 2014 vilifikia 385 kutoka 240 vyamwaka 2013. Sababu kwabwa yaongezeko hili ni ukosefu wa hew asafi, malaria kali na maambukizo ya magonjwa mengine.
 

 mkuu wa wilaya Lindi Fatma Ali akizungumza na wananchi kwenye siku ya eco bank mkoani mtwara
Watoto na eco bank Mtwara

Post a Comment

 
Top