0
 Wapiga kura
 Wapiga kura wamekuwa wakikagua maelezo kuwahusu kwenye sajili ya wapiga kura vituo vya kupigia kura
Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania imetoa takwimu kuhusu wapiga kura wanaotarajiwa kushiriki uchaguzi mkuu Jumapili Oktoba 25.
Takwimu hizo zinaonyesha mikoa yenye kura nyingi pamoja na kiwango cha walizo nazo wanawake na vijana.
Idadi ya vijana waliojiandikisha kupiga kura inaonyesha mgombea atakayekuwa na nafasi nzuri ya kushinda ni atakayeweza kuvutia kura za vijana.
Idadi ya wapiga kura kwa mujibu wa mikoa
Na Mkoa Idadi ya wapiga kura
1 Arusha 1,009,292
2 Dar es Salaam 2,775,295
3 Dodoma 1,071,383
4 Geita 887,982
5 Iringa 529,887
6 Kagera 1,051,681
7 Kaskazini Pemba 11,570
8 Kaskazini Unguja 9,601
9 Katavi 322,127
10 Kigoma 792,551
11 Kilimanjaro 800,349
12 Kusini Pemba 8,986
13 Kusini Unguja 5,077
14 Lindi 514,558
15 Manyara 678,586
16 Mara 892,741
17 Mbeya 1,397,653
18 Mjini Magharibi 12,948
19 Morogoro 1,271,951
20 Mtwara 728,981
21 Mwanza 1,448,884
22 Njombe 383,366
23 Pwani 697,533
24 Rukwa 459,573
25 Ruvuma 739,774
26 Shinyanga 773,273
27 Simiyu 718,777
28 Singida 648,897
29 Tabora 1,097,760
30 Tanga 1,009,753
JUMLA
22,750,789
Eneo la Unguja lina wapiga kura 358,180 na Pemba 145,013, jumla ya wapiga kura visiwani Zanzibar ikiwa 503,193.
Kwa jumla, wapiga kura wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni 23,253,982.
Takwimu hizo zinaonyesha wapiga kura wanaume ni asilimia 47 na wanawake asilimia 53, ikiwa na maana kwamba wanawake ni wengi kushinda wanaume katika sajili ya kura.
Wapiga kura vijana walio na umri wa kati ya miaka 18 na 35 ni asilimia 57 ya wapiga kura wote.
Wapiga kura walio na umri wa zaidi ya miaka 50 ni asilimia 18 pekee, hao wengine asilimia 25 wakiwa na umri wa kati ya miaka 36 na 50. BOFYA  HAPA

Post a Comment

 
Top