Ukame
Mashirika ya
misaada yanasema watu robo ya milioni wanaathirika kutokana na ukame
katika eneo lililojitangazia uhuru la Somaliland.
Mashirika hayo
yanasema utapia mlo umeathiri watu vibaya hasa watoto wa chini ya miaka
mitano. Watu kumi na watatu wameripotiwa kufa.Kulingana na mashirika hayo asilimia arobaini ya mifugo imekufa kutokana na ukosefu wa maji na uhaba wa chakula.
Familia zinalazimika kuishi bila vyakula vya kutosha , kunywa maji machafu na kuhamahama kutafuta chakula.
Maeneo yalioathirika zaidi ni yale ambayo huzalisha chakula kwa kiwango kikubwa.
Post a Comment