0



1.DIRA-Kuwa na dira ni kujua unapoelekea na kuwa tayari una picha halisi ya maendeleo yako kichwani.Dira inatakiwa kiwe kitu ambacho kinawezekana kukamilishwa na kila mmoja kwenye kundi.
Kiongozi:unaweza ukaona wazo la dira yako likitekelezeka ,unaweza kuwasilisha dira na malengo yako kwa hatua rahisi na ndogondogo kwa wanakikundi wenzako wakakuelewa.
Mfuasi:unahitaji  kuelewa na kukubaliana na dira ya kikundi na pia kuelewa kazi zinazohitajika kufanyira na malengo hakuwezi wa ili kufanyikisha hilo.Pale kila mmoja atakapoweza kuelezea dira kwa namna moja ,ndipo inakuwa dira ya pamoja ,hii itakupa motisha na kuongoza vitendo vyenu.
2.kujituma na kujitoa-kufikia na malengo hakuwezi kuja kwa kasi kama kumba na kufungua macho,la hasha ,inahusisha kazi kubwa  na ya muda mrefu.kujituma na kujitoa kuna maanisha kutoa muda ,nguvu na ujuzi wako kufikia malengo.
Kiongozi:ni lazima ujitume na kujitoa kw amalengo yako,wafuasi wako wanajituma zaidi na kufanya kazi yenye matokeo bora ukiongoza kwa mfano,kiongozi mzuri anafanya kuhudumia wafuasi wake na si kwa faida yake binafsi.
Mfuasi:unatakiwa ujitoe kama kiongozi anavyojitoa ,umejipanga na kujiandaa kutoa mawazo na muda wako  kusaidia kundi zima kufikia dira yenu.
3:Kujiamini:ni  kuwa na imani kwamba kitu kiko sahihi na uamuzi uliofanywa ndiyo sahihi na bora zaidi,kuamini kwamba anaweza kutenda kazi yake kwa ufanisi.Ili kuweka mwelekeo,kiongozi anahitaji kuonekana uwezo wake akiwa ametulia katika nafasi yake .Hii inawahamasisha WENGINE
KUJIAMINI na kutoa msaada wa kuhakikisha kiongozi anafanyikiwa .
Kiongozi:Ili kuweka mwelekeo ,kiongozi unahitaji kuonekana unajiamini kuhusu uwezo wako na unaiweza nafasi yako unatakiwa uwe na unyenyekevu wa kusikiliza maoni ya wengine,kukiri unapokosea na kutambua hekima ya wengine.
Mfuasi:unatakiwa uwe na imani na kiongozi na uelewe kwamba wote mnafanya kazi kuelekea lengo mojdilifua lakini uaminifu wako usiwe bila kipimo ,unatakiwa ujiamini kiasi cha kusimama  na kuzungumza pale unapoona kiongozi amekosea au unapoona kunafanyika kitu kinyume cha maadili.
4;Mawasiliano-kitu cha muhimu kujua kuhuisu  mawasiliano ni kwamba huo ni mchakato wa njia mbili,kusikiliza ni muhimu kama ilivyo muhimu kuzungumza. Kuwafanyawatu wote wafanye kazi pamoja unahitaji kushirikisha wengine juu ya dira na malengo kwa uwazi na kueleza kile ambacho kinahitajika kufanyika. Mawasiliano mazuri yanasaidia kila mmoja kujifunza kutokana na makosa na kuweza kwenda mbele.
Kiongozi:Unahitaji kutoa taarifa kuhusu uamuzi na kutoa mwongozo na kueleza vizuri juu ya ubnachotaka kifanyike.Unahitajikuwapa moyo na msaada wanaokuzunguka .
Mfuasi;Unaweza kuzungumza na kiongozi na wafuasi wengine.  Viongozi wanahitaji mtu wa kuwaambia mambo yanayokwenda vizuri na yale yanayokwenda kombo,ili waweze kufanya uamuzi bora.
5.Uadilifu:Uadilifu maana yake ni kufuata kanuni za maadili. Uaminifu ni sehemu muhimu ya uadilifu na ukiwa mwadilifu unaweza kuaminiwa kw          a sababu kamwe hutaliweza kukiuka maadili na hata wakati ambao yanaweza kuwanufaisha wenyewe. Kwa mfano, mtu mwadilifu hawezi kuchukuwa rushwa.
Kiongozi:Ni mkweli na muwazi kwa wafuasi wake. Utaaminika kwa sababu unatenda unachosema.lazima pia uwe mwangalifu na mahitaj ya watu wengine.mamlaka ya kweli huzaliwa kutokana na heshima,tabia njema na uaminifu kwa kila mtu ambaye unamuongoza.
Mfuasi.. Kiongozi anahitaji kukuamini kwamba unafanya kile unachotakiwa kufanya, anakuaminia. Uadilifu huendeleza tabia na hujenga uwajibikaji ,uwazi na uaminifu. Hii ni misingi ya kukujenge heshima kutoka kwa wale walio karibu yako au unaowaongoza , ikiwa ni pamoja na wanafunzi wenzanko, wanatimu wenzanko au hata wapiga kura wako.
6. Uwajibikaji : uwajibikaji ni kuwa mkweli kwa wale unaowawakilisha. Pia ni wajibu wa kila mmoja, viongoz na wafuasi,kuhifadhi na kuripoti shuguli zao, kukubali wajibu wao na kutoa matokeo katika njia ya uwazi. Hii vilevile, inahusisha wajibu wa matumizi ya fedha au mali nyingine.
Kiongozii: unawajibika na unatakiwa ujitahidi kupata matokeo bora kutokana na utendaji wako, pia kuchukua hatua zaki uwajibikaji pale kundi zima linaposhindwa kutimiza wajibu bila kujali makosa gani yamefanyika.
Mfuasi: unatakiwa kuchukua umiliki kamili wa majukumu yako na uwasaidie wenzako’ ukijua kuwa mafanikio ya kundi hayawezi kuzidi yale ya mmoja wao alie mtendaji dhaifu kuliko wote!
WATU WENGI SI VIONGOZI WAZURI NA WENGINE WALA HAWATAKIWI KABISA KUWA VIONGOZI ,ILA WANAWEZA KUWA WAFUASI WAZURI VIONGOZI BORA WANAITAJI WAFUASI BORA

Post a Comment

 
Top