Shirikisho la soka
nchini Uingereza FA limeweka mfano mbaya kwa kubadilisha uamuzi wa kadi
nyekundi aliyopewa beki wa Arsenal Gabriel Paulista kulingana na kocha
wa Chelsea Jose Mourinho.
Beki Gabriel Paulista alipigwa kadi
nyekundu kwa kumpiga teke Diego Costa wakati Chelsea ilipoibuka mshindi
kwa mabao 2-0 dhidi ya Arsenal katika mechi ya ligi kuu ya Uingereza
siku ya jumamosi.Costa alipigwa marufuku kwa kuzua ghasia katika kisa na beki mwenmgine wa Arsenal Laurent Koscielny kilichosababisha Gabriel kupigwa kadi nyekundu.
Mourinho alisema kuwa hakuzungumzia swala la kupigwa marufuku ya mechi tatu kwa Costa kwa hofu ya kupewa marufuku.
Post a Comment