0


 

 Na mwaandishi wetu 
CHAMA cha wananchi (CUF) taifa kimekabidhi msaada wa bati 60 pamoja na vifaa mbalimbali vya ujenzi vyenye thamani ya Sh.milioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Mpulima iliyopo katika kata ya Mbuyuni Halmashauri ya wilaya ya Masasi mkoani hapa.
Akikabidhi msaada huo juzi kijijini hapo kwa uongozi wa shule hiyo kwa niaba ya mwenyekiti wa Chama hicho taifa,Prof.Ibrahim,Lipumba,mkurugenzi  wa mipango na uchaguzi taifa,Shaweje Mketo alisema kama kawaida Chama cha CUF kinaendelea kutathamini na kutatua huduma za msingi wanazozikosa wananchi.
Alisema msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya mwenyekiti wa Chama hicho taifa Prof.Ibrahim Lipumba aliyoitoa mapema mwaka huu baada ya kufanya ziara katika shule hiyo na kukuta hali ya madarasa yakuwa kwenye mazingira magumu na baadhi ya wanafunzi wakisoma chini miti kwa kukosa vyumba vya madarasa.
Mketo alisema kuwa licha ya Chama hicho kuwa na uwezo mdogo wa kifedha lakini kinaona upo umuhimu wa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi kwakuwa serikali iliyopo madarakani imeshindwa kuwatatulia changamoto hizo.
Alisema kutokana na wanafunzi wa shule hiyo kukosa miundombinu rafiki ya vyumba vya madarasa Chama cha wananchi (CUF) kimeamua kutoa msaada huo wa bati 60 pamoja na vifaa vingine vya ujenzi ikiwemo misumari vizibo vya kugongea bati.
“Sisi kama Chama cha wananchi CUF tumeguswa na tatizo hili la shule ya msingi Mpulima ndio maana tumechukua jukumu la kutoa msaada huu wa bati ili kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa ii watoto hawa wasienelee kusomea chiti miti,”alisema Mketo
Alisema Chama hicho kinataendelea kutoa misaada mbalimbali ya kijamii ili kuhakikisha wananchi wanaondokana na changamoto zinazowakabili ambazo serikali ya CCM imeshindwa kuzipatia ufumbuzi kutokana na viongozi wake kutojali matatizo ya wananchi.
Aidha Mketo kwa niaba ya Chama hicho alitoa fedha sh.150,000 kwa ajili ya mafundi watakaotengeneza vyumba hivyo vya madarasa ili jitihada hizo za matengenezo zifanyike kwa haraka hatimaye wanafunzi waweze kusomea madarsa hayo haraka.
Akipokea msaada huo mwalimu mkuu wa shule hiyo Semeni Nyumayo alikipongeza Chama hicho kwa kutoa  msaada huo wa bati  na kueleza kuwa awali wanafunzi wake walikuwa wakisomea chiti ya miti kutokana na ukosefu wa vyumba vya madarasa.                          
Alisema shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 599 wa kuanzia darasa la kwanza hadi la saba na kwamba kwa muda mrefu wanafunzi wa darasa la sita walikuwa hawana chumba cha darasa na kuanzia sasa vyumba hivyo viwili vitakamilika na wanafunzi hao wataondokana na adha hiyo ya vyumba vya madarasa.

Post a Comment

 
Top