Na mwaandishi Wetu
MILA na desturi za Jando
na unyago zinazofundishwa kwa vijana katika mikoa ya Lindi na Mtwara zimetajwa
kuwa ni sababu moja wapo ya kuwepo kwa mimba za utotoni pamoja na maambukizi ya
ukimwi kwa vijana kwenye mikoa hiyo.
Hayo yalielezwa jana na
katibu wa shirika lisilo la kiserikai la maendeleo Masasi (MADA) Bernedetha
Jumla alipokuwa akizungumza na kikundi cha vijana cha juhudi kilichopo katika
kijiji cha Sululu Halmashauri ya mji Masasi mkoani humo.
Alisema kuwa mashirika
yasiyo ya kiserikali ya GIZ,EVERPLAN,DSW,yalifanya utafiti katika wilaya za
mikoa hiyo ikiwemo ya Masasi na kwamba matokea ya utafiti huo yalibaini kuwa
baadhi ya changamoto zilizopo ikiwemo mimba za utotoni pamoja na
maabukizi ya ukwimi zinasababishwa na mila na desturi zinazofundishwa kwa
vijana katika jando na unyago.
Katibu huyo alisema
kufuatia matokea hayo ya utafiti ilipelekea shirika la MADA liliamua kubuni
mradi wa afya ya uzazi na jinsia kwa vijana lengo la mradi huo ni kuwafanya
vijana wabadili tabia zao ikiwemo ngono uzembe ambazo uchangia mimba za utotoni
pamoja na maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.
Alisema vijana waliohusishwa
katika mradi huo ni wenye umri wa miaka 14 hadi 24 na kwamba mradi huo ni wa
miezi sita na unafadhiliwa na mashirika ya DSW,EVERPLAN na GIZ kutoka
Ujerumani, hivyo hatua ya kwanza ambayo imefanyika ni mafunzi ya kuwajengea
uwezo viongozi wa shirika hilo ili weweze kutekeleza mradi huo kwa ufanisi
zaidi.
Jumla alisema pia
wamehamasisha vijana juu ya uanzishwaji wa vituo vya klabu za vijana katika
Halmashauri mbili ya mji Masasi na Halmshauri ya wilaya ya Masasi na kwa sasa tayari
wameshaunda klabu mbili zenye vijana 25 kila moja katika ngazi ya kata na
kijiji kwenye kila Halmashauri.
Alisema kwa sasa
wameanza na vikundi viwili ambapo ni kikundi cha Juhudi kilichopo kijiji cha
Sululu Halmashauri mji Masasi na Kazi moja kijiji cha Mihima Halmashauri ya
wilaya Masasi,juhudi wanajishughulisha na kilimo pamoja na ufugaji huku Kazi
wao wanajishughulisha na ufugaji wa nyuki,kuku na masuala ya kisanii.
“Tutahamasisha
Halmashauri za mji na wilaya ya Masasi ziingize mpango kazi wa elimu ya afya ya
uzazi na jinsia kwa vijana na zipangiwe bajeti ili AZISE zitekeleze kila mwaka
mipango hiyo,”alisema Jumla
Aliongeza kuwa bado
mwamko wa vijana kujitolea kushiriki katika shughuli za kimaendeleo ni mdogo
hivyo wanahitaji kuelimishwa zaidi aidha uwelewa wa elimu ya afya ya uzazi na
jinsia kwa vijana ikiwemo na uhamasishaji pia unahitajika katika jamii.
Post a Comment