0


SIKU YA HAFLA MAALUM KWA WALEMAVU ILIYOFANYIKA WILAYANI LIWALE MKOANI LINDI SIKU YA TAREHE 29/3/2015 (PICHA KWA HISANI YA MDAU WETU)
Na mwandishi wetu Liwale-Lindi
Kitengo cha ustawi wa jamii,wilaya Liwale mkoa wa Lindi kimakabiliwa na changamoto mbalimbali ikwemo kutokuwa na bajeti ya fedha hali inayofanya washindwe kufika vijijini ili kutathimini matukio ua vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.
Hayo yamebainisha kwenye hafla maalum kwa ndugu zetu wenye ulemavu iliyofanyika wiki iliyopita tarehe 29/3/2015 na ofisa ustawi wa jamii  wilaya Liwale Freddy Magelasa kwenye Tafrija ya watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na mkuu wa wilaya hiyo .
 Magelesa alisema  changamoto kubwa  inayoikabili kitengo cha ustawi wa jamii wilayani humo  katika kutekeleza majukumu yake ni ukosefu wa fedha kwa ajili yakusimamia na kutekeleza   wa kazi hizo.
Jamii inatulaumu kwa kutofika kwenye matukio ,ukweli mazingira si rafiki, kutokana  na kukosa fedha za uendeshaji alisema Magelesa.
Kwa upande wake katibu wa chama walemavu wilaya Liwale Saidi Jika alisema matukio ya,kunyanyasika,walemavu akina mama na watoto,kubakwa na kutelekezwa kimajukumu yamekuwa yakijitokeza kila wakati kutokana na jamii kutoelewa athari za matuki hayo kwa sasa na siku za usoni na kuiomba serikali kuyatafutia ufumbuzi

Post a Comment

 
Top