0

HOSPITALKaunti ya Elgeyo Marakwet nchini Kenya inakabiliwa na changamoto kubwa ya wauguzi katika kituo cha Afya cha Simbeiwe, lakini changamoto hiyo inatokana na ishu ambayo imelalamikiwa sana na wahudumu wa afya ambao huwa wanapelekwa maeneo hayo.
Wahudumu wanaopangiwa kufanya kazi katika kituo hicho wanalalamika kwamba eneo hilo lina matukio ambayo yanahusishwa na imani za kishirikina.
Mmoja wa wauguzi aliyeacha kazi katika kituo hicho anasema alikutana na maajabu ya zimwi lililomning’iniza mtoto mdogo hewani bila kumshika wakati alipokuwa akijitayarisha kumchoma sindano mtoto huyo.
Waziri wa Afya katika kaunti hiyo, Thomas Ruto amesema wanatafuta wahudumu wa afya ambao wataweza kuhimili kazi katika mazingira kama hayo.
Kiongozi mwingine amepingana na taarifa kwamba kuna ishu ya uchawi kuwepo maeneo hayo, anasema uchawi ulikuwepo zamani ila kwa sasa haupo.

Post a Comment

 
Top