Huku
nusu ya matokeo katika uchaguzi wa rais nchini Nigeria yakiwa
yametangazwa, mgombea kutoka chama kikuu cha upinzani, Muhammadu Buhari,
anaongoza dhidi ya rais aliye madarakani, Goodluck Jonathan.
Lakini
majimbo ya kusini yenye idadi kubwa ya watu kama vile Lagos na Rivers
bado hayajatangaza matokeo na mwandishi wa BBC mjini Abuja amesema
mchuano bado ni mkali.
Tume
ya uchaguzi imesema itaendelea kutangaza matokeo ya uchaguzi Jumanne
asubuhi na kwamba matokeo ya mwisho yanatarajiwa kutolewa baadaye siku
hiyo. Mwandishi wa BBC anasema yeyote atakayeshinda, litakuwa jambo la
kushangaza iwapo mgombea atakayeshindwa hatatamka kuwepo kwa mbinu
chafu.bbc swahili
Post a Comment