0
 
Licha ya wadau wa habari kuwasilisha ombi kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda wakitaka miswada miwili ya habari ya mwaka 2015 iwasilishwe kwa mfumo wa kawaida, Serikali imeing’ang’ania huku ikisema itawasilishwa chini ya hati ya dharura Jumanne ijayo.
Miswada hiyo ni kati ya minne yenye ‘utata’ ambayo ilikuwa iwasilishwe bungeni leo na kesho, lakini jana ofisi ya Bunge ilitoa ratiba mpya inayoonyesha kuwa itawasilishwa wiki ijayo chini ya hati ya dharura, ikiwa ni kinyume na maombi ya wadau wa habari.
Kaimu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu aliliambia gazeti hili jana kwamba Serikali inataka kufanya ubabe na imepanga kuiwasilisha Jumanne asubuhi licha ya wabunge kutojua nini kimeandikwa.
Miswada hiyo ni pamoja na ule wa Sheria ya Miamala ya Kielektroniki wa mwaka 2014, Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao wa mwaka 2015, Muswada wa Sheria ya Kupata Habari wa mwaka 2015 na Muswada wa Sheria ya Vyombo vya Habari.
Juzi, wadau hao walimwomba Spika Makinda atumie hekima kuishauri Serikali iiwasilishe katika mfumo wa kawaida miswada miwili ya habari, ili kutoa fursa kwa wananchi na wadau kutoa maoni kabla ya kupitishwa na kuwa sheria.
Imeelezwa kuwa Jumanne, Muswada utakaoanza kuwasilishwa bungeni ni ule wa Sheria ya Kupata Habari na utafuatiwa na wa Sheria ya Vyombo vya Habari.
“Tunajua kuwa miswada hii imelenga kuvifungia vyombo vya habari, maana huu ni mwaka wa uchaguzi. Wanachokifanya Serikali ni kuiwasilisha bungeni ‘kimafia’ tu. Sisi tutakachokifanya ni kuibana bungeni,” alisema Lissu.
Hata hivyo, alisema kutokana na wingi wa wabunge wa CCM, huenda miswada hiyo ikapitishwa, jambo alilodai kuwa litakuwa gumu kulizuia.
“Mpaka sasa hatujaipata miswada hii, kwa kweli jambo hili linatusikitisha maana hata katika kamati haijafika,” alisema Lissu.
Tangu mkutano wa 19 wa Bunge unaoendelea mjini hapa ulipoanza, kumekuwa na taarifa kuwa Serikali inakusudia kuwasilisha miswada hiyo chini ya hati ya dharura, lakini wadau wa habari wameendelea kuiomba ibadili msimamo huo kwani kufanya hivyo kutawanyima wananchi fursa ya kutoa maoni juu ya miswada hiyo kabla ya kuwa sheria.
Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel juzi alilieleza gazeti hili kuwa miswada hiyo hata ikiwasilishwa itakuwa vigumu kujadiliwa kutokana na muda uliopo, huku akishindwa kuthibitisha kama kweli itawasilishwa ama laa.
Alipotafutwa tena jana, Kaimua Katibu huyo wa Bunge, Joel kufafanua mabadiliko ya ratiba hiyo na kama miswada hiyo pamoja na hati ya dharura vimeshafikishwa katika ofisi ya Spika, hakupatikana.KUENDELEA BOFYA HAPA
inakusudia kuwasilisha miswada hiyo chini ya hati ya dharura, lakini wadau wa habari wameendelea kuiomba ibadili msimamo huo kwani kufanya hivyo kutawanyima wananchi fursa ya kutoa maoni juu ya miswada hiyo kabla ya kuwa sheria.
Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel juzi alilieleza gazeti hili kuwa miswada hiyo hata ikiwasilishwa itakuwa vigumu kujadiliwa kutokana na muda uliopo, huku akishindwa kuthibitisha kama kweli itawasilishwa ama laa.
Alipotafutwa tena jana, Kaimua Katibu huyo wa Bunge, Joel kufafanua mabadiliko ya ratiba hiyo na kama miswada hiyo pamoja na hati ya dharura vimeshafikishwa katika ofisi ya Spika, hakupatikana.

Post a Comment

 
Top