1. Ernest Wendeleni, Chikunja.
Hakuna zahanati Chikunja, uliahidi utajenga mpaka leo kimya. ?
Jibu: Kwanza niseme kuwa Ernest hajafika Chikunja
kwa zaidi ya miaka mitano. Chikunja kuna zahanati inafanya kazi kwa
zaidi ya miaka mitano sasa na wananchi wanapata huduma. Hata hivyo
tutaendelea kuhakikisha huduma za afya zinakuwepo na zinapatikana kama
ilivyopangwa.
2. Hassan Hassan Misinzo, Ndanda.
Uliahidi utahakikisha kuna mashine za kusaga mpaka sasa hakuna. Kwa nini hukutimiza ahadi hiyo?
Jibu; Katika ahadi zangu wakati nagombea sijawahi
kuahidi mashine za kusaga. Kama wana shida ya mashine za kusaga waseme
wasaidiwe.
3. Hassan Mpalanga. Masasi Mjini.
Hakuna vituo maalumu vya usafiri katika maeneo mengi, lini utabadilisha mandhari ya mji wa Masasi iwe ya kupendeza?
Jibu:Tuna stendi kuu ya mabasi Masasi mjini,
ambayo ina kituo kikubwa cha mabasi ya mikoani na ya ndani. Hata hivyo
tumeshatengeneza eneo la kujenga stendi kubwa kwa sababu kuna ongezeko
kubwa la watu na maendeoe. Eneo hilo lipo karibu na uwanja wa ndege.
4. Prisca Mlaponi, Nagaga.
Hospitali ya Nkomaindo bado inakabiliwa na
uhaba wa dawa na vitanda. Uliahidi tatizo hilo litakwisha. Vipi mpaka
sasa unatusaidiaje?
Jibu: Ni kweli kulikuwa na uhaba wa vitanda na
dawa, nilitafuta wafadhili, nikapeleka vitanda na magodoro. Magodoro ya
‘ICU’ yalinunuliwa ili kusaidia wagonjwa mahututi lakini ieleweke kuwa
suala la dawa ni tatizo la nchi nzima. Nimejitahidi kufanya vikao na
halmashauri ili kuhakikisha kuwa fedha zinazipatikana zinunue dawa
muhimu. Nilimueleza Rais kuhusu tatzo hili, alitoa muongozo kutatua
hilo. Sisi viongozi tunalifanyia kazi bado.
5.Deniss Chimwaga, Liwale
Kwa nini umeme mpaka sasa haujafika katika maeneo mengi. Huoni kuwa uchumi wa Masasi utaimarika kama umeme utakuwepo?
Jibu: Nilipoingia madarakani, umeme ulikuwepo
katika maeneo ya mijini tu. Lakini kwa kipindi nilichokaa madarakani
umeme umeendelea kuwepo katika maeneo mengi kwa kupitia wakala wa umeme
vijijini, REA. Hata hivyo umeme utaingia vijijini hatua kwa hatua, umeme
utawekwa kama nilivyoahidi. Alipokuja Rais Jakaya Kikwete na Nape
Nnaye, nilitoa wazo, kuwepo kwa programu maalumu ya kusambaza umeme
vijijini, wananchi watashindwa kuelewa kuwa gesi imewanufaishaje.
Niliomba pia katika ilani ya CCM, Masasi ipewe kipaumbele kupata umeme.
6. Christopher Saimon Mtambalike, Chigugu.
Ufaulu ni mdogo sana shule za Masasi, mimba za utotoni zimekithiri na elimu ni duni kwa ujumla. Utaliondoaje tatizo hili?
Jibu; Ni kweli kabisa. Sababu ya elimu duni ni
kwanza changamoto kutoka kwa wazazi kutowaandaa watoto kielimu. wapo
tayari kuwasomesha watoto hadi darasa la saba tu, baaada ya hapo
hawataki. Kuna shule za kata maeneo mengine kuna shule mbili lakini
wazazi wanakataa kuwapeleka watoto. hawafanyi mandalizi mazuri kwa
watoto. Lakini pia kuna upungufu wa walimu suala ambalo nimelipeleka
wizarani na wananisaidia. Kuna upungufu wa madarasa lakini fedha za
mfuko wa jimbo zimesaidia. Wazazi wapo tayari kuchangia harusi, unyago
wa kifahari lakini kupeleka watoto shule wanakuwa wagumu. Viongozi
wanahamasisha na kujenga shule za sekondari, msingi na vyuo lakini bado
kuna tatizo kwa wazazi.
7. Alfred Mitande, Liwale.
Wanafunzi wengi wanatumikishwa kazi wakiwa
shuleni hali inayosababisha washindwe kufanya vizuri kwenye masomo. Je,
utatusaidaje kuondoa tatizo hili.
Jibu; Hata sisi zamani tulikuwa tunafanya kazi
shuleni na elimu ilikuwa juu. wazazi wa sasa hawataki watoto wafanye
kazi. leo hii ni shule chache zenye mashamba. Zamani ilikuwa tunalima
shamba la shule halafu tunapata chakula shuleni hapo hapo. Ninatembelea
shule na kufanya vikao hilo ni tatizo ni dogo sana. lakini kwa sasa
wazazi hawataki hilo, wamebadilika hivi kweli mwalimu atashindwa kumtuma
mwanafunzi ndoo ya maji. Kazi nyingine ni sehemu ya wajibu wao.
8. Anna Martin, Chikunja.
Uliahidi visima katika vijiji vyote vya masasi na kuwa tatizo la maji litapungua. Vipi mpaka leo hakuna matokeo chanya.
Jibu; Nilipoingia madarakani kulikuwa na shida ya
maji kuanzia mijini hadi vijijini. Ndoa zilikuwa mashakani, lakini hilo
tatizo limepungua kwa kiasi kikubwa. Nina mradi wa maji Liwale
ukikamilka utasaidia vijiji vitatu ambavyo ni Lilala, Muungano na
Nanyindwa. Kuna mradi upo tayari kijiji cha Mtakuja wananchi wanapata
maji. Kuna mradi Nambawala Nanganga, Ndanda, Chipute na Nkwera kote
miradi inaendelea kuwasaidia wananchi wapate maji. Mradi ukikamilka
utahudumia vijiji hivyo. Kuna miradi ya mabwawa huko Muungano na
Chiwale. Hizo zote ni jitihada kuhakikisha jimbo langu linapata maji.
9.Happiness Namulimuka, Liwale.
Usafiri wa bodaboda unatumika kufanya matukio mengi ya uhalifu wilayani Masasi, je, utaliutatuaje hili?
JIBU; Bodaboda zinawasaidia wananchi kuanzia mjini
na vijijini, kama zinatumika katika uhalifu, hilo suala ni la kiusalama
zaidi. Sijawahi kupokea malalamiko hayo kwangu na kama wanapeleka
malalamiko polisi basi wanapeleka sehemu sahihi. Hata hivyo nitazungumza
na mkuu wa mkoa na kupata ukweli, kama ni kwli zitafanyika jitihda za
kuondoa tatizo.
10.Victor Kasembe, Masasi Mjini.
Hatukusikii mara kwa mara bungeni ukiwatetea wananchi wako kama wabunge wengine. Je, tutakupaje kura kwa msimu huu?
Jibu; Nafikiri Victor husikilizi kipindi wala
hufuatilii. Ninayo orodha ya maswali ninayouliza bungeni. Zipo rejea za
maswali na michango yangu na nina orodha ya kila kitu ninachofanya
bungeni. Sikurupuki kuzungumza mambo ambayo si ya msingi. Maendeleo haya
yote nimeyapata kupitia michango yangu na maswali ninayoyatoa bungeni.
Victor nakuomba unipe kura yako ili niendelee kuzishughulikia kero
nyingine zilizopo Masasi.
Post a Comment